87
1. Mwisho wa njia ya mkristo ni mbinguni; Yesu ananiongoza salama. Kama shetani akinijaribu nakitazamia kifiko.
Pambio:
Kwetu mbinguni hatutatawanyika, dhambi na mateso hayatakuwapo, Na hatutaona machozi na shida, ila furaha milele.
2. Tutawaona walioishinda dhambi, shetani na mambo mabaya, na tutaona Mwokozi mpenzi; tutafananishwa na yeye.
3.Nani ataka kufika mbinguni? Yesu ni njia, uzima na kweli. Njoo kwa Yesu! Akuandalia kao la milele mbinguni.
4. :/: Malaika wanangoja:/: malaika wanangoja huko mbinguni! :/: Malaika wanangoja:/: kutusalimu: «karibu».