Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

233 TAZAMA Mwokozi aliekufilia

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

233

1. Tazama Mwokozi aliyekufilia ili wewe upate uzima! Tazama, kwa pendo atakusaidia, usidumu dhambini daima!

Pambio:
Yainue macho! Tazama Mwokozi aliyekufilia, ili upate uzima!

 

2. Mwokozi alisulibiwa ju’ ya mti ili sisi tupate wokovu. Alitukomboa kwa damu yake safi, kwate yeye twapata wongofu.

 

3. Hakuna majuto yaweza’ kutuponya, ila damu ya Yesu Masiya. Ufike kwa Yesu apate kukuonya jinsi yaondokavyo hatia!

 

4. Rafiki, waitwa na Mungu kwa wokovu, anataka ufike upesi. Kwa nini kukawa, ufike bila hofu, uondoke katika hatari!

 

5. Ufike, pokea uzima wa milele, Bwana Yesu ali’tuletea! Karama ya mbingu ni tumaini letu, ipokee na hutapotea!

Amelia M. Hull, 1860

No comments yet.

Leave a Comment