222 BWANA Yesu amesema

1.Bwana Yesu anasema: “Dhaifu wewe sana. Mimi ni mchunga mwema”. Na kwa hiyo namwandama.

Pambio: Yesu alikufa kwa ajili yangu, aliziondoa dhambi, furaha kubwa kwangu!

2.Pendo la Mwokozi wangu limeyeyusha moyo. Ametoa dhambi zangu na kiburi na uchoyo.

3.Sina kitu mkononi cha kunifaidia; udhaifu u moyoni, Yesu ninamlilia.

4.Mungu akisaidia nitamaliza mwendo. “Yesu alinifilia”, nitaimba huko ng’ambo.

5. Siku moja nitafika mbinguni huko juu, nitaimba kadhalika shukrani kuu.

Elvina M. Hall- T.Truvé
Min Jesus säger mig, Sgt. 419; I hear the Saviour, R.H. 198




7 MWOKOZI ameutimiza wokovu kwa neema kubwa

1. Mwokozi ameutimiza wokovu kwa neem kubwa,
Na juu ya mwamba wa Neno la Mungu Najenga imani.

Refrain:
Aliniokoa kabisa! Kwa damu alinisafisha.
Ninamshukuru Mwokozi kwa sababu Alinikomboa hakika ! 

 

2. Mzigo wa dhambi aliuondoa kwa neema kubwa.
Naona Furaha rohoni kabisa, Amani ya Mungu. 

 

3. Naweza kukaa mweupe rohoni kwa neema kubwa;
Na roho ya Mungu ananiongoza Njiani daima. 

 

4. Karibu na Yesu nalindwa salama Kwa neema kubwa.
Ahadi za Mungu zanipa Furaha iliyo kamili.


 




32 HAPO nilikua chini katika dhambi nyingi

32

1. Hapo nilikuwa chini Katika dhambi nyingi, roho yangu iliona kufa na giza tele. Mungu alikisikia kilio changu huko, naye akanipandisha, kuniponya.

Pambio:
:/: Nimeokoka, nimeokoka! Yesu Mwokozi wangu aliniokoa:/:

2. Sasa Yesu amekuwa makimbilio yangu, na upendo wake ‘kubwa uko moyoni mwangu. Ne’ma yake kubwa sana inajaliza roho, niwe mwaminifu kwake siku zote!

3. Ewe, mwenye sikitiko, kuna matumaini: Yesu anakufahamu, atakusaidia. Atakupandisha toka tope la kuteleza, upokee ne’ma yake kwa wokovu!

James Rowe, 1912




34 KWA pendo lake kubwa alitafuta mimi

34

1. Kwa pendo lake kubwa alitafuta mimi, na alinichukua begani mazizini na nyimbo zao malaika zikajaza mbingu pia.

Pambio:
Alinitafuta, akaniokoa, akaniondoa matopeni, akanichukua mazizini.

2. Mchunga mwema Yesu aliniponya roho, na akaniambia: «Mtoto upendwaye». Sauti yake ya upendo ikaufariji moyo.
3. Ninakumbuka jinsi alivyotoka damu, na taji ya miiba, mateso ya mauti. Na penye msalaba wake ninashukuru Bwana Yesu.
4. Namfuata yeye katika nuru yake, waridi za ahadi zapamba njia yangu. Milele nitaendelea kusifu Yesu kwa furaha
5. Na saa zinapita, nangoja asubuhi utakaponiita, niende kwako juu. Nitasimama kwa amani mbinguni mbele yako, Yesu.

W. Sencer Walton




36 YESU ameniokowa

36

1. Yesu ameniokoa, amenipa utulivu. Kwake ninaona raha, ninataka kumsifu.

Pambio:
Haleluya, haleluya! Nimefika bandarini. Haleluya, haleluya! Jina lake ni mnara.

2. Kwa furaha ninaimba wimbo mpya wa wokovu. Nisichoke kamwe hapa kumwimbia Mkombozi.

3.Ni habari za neema zakupasha pande zote. Mhubiri, enda mbio kufikia nchi zote!

4. Yesu, siku nita’kufa na maisha ni tayari, ‘nichukue kwako juu penye raha ya milele!

S.L. Oberholzer, 1885

 




37 BWANA Yesu aliniokoa kweli

37

1. Bwana Yesu aliniokoa kweli, ninataka kufuata yeye sasa. Kila siku nimtumikie vema, yeye anipaye roho kwa neema!

Pambio:
Nafuata njia nzuri ya Mfalme Yesu Kristo, Na katika njia hiyo Mwendo ni pamoja naye.

 

2. Sitaifuata njia mbaya tena, nimewekwa huru kweli naye Yesu. Kumtumikia ni furaha yangu, ananishibisha kwa fadhili zake.

 

3. Huko mbele ninaona mji mwema, nimeacha njia ndefu nyuma yangu. Nuru ya Babangu yaniangazia, nitembee kwa salama siku zote.

 

Henri Dixon Loes




38 NILIKWENDA mbali sana

38

1. Nilikwenda mbali sana, ‘kufuata njia mbaya, nikamsahau Yesu anayenipenda sana.

Pambio:
Nina raha na furaha, Yesu alinitafuta, akaniokoa kweli, mimi wake siku zote.

 

2. Na sikufikiri siku nitakapodhihirishwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na kuhukumiwa naye.

 

3. Dhambi zilinichokesha, nikageukia Mungu, akasema neno nzuri la amani na furaha.


Original Version:

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=bkB7V8GUGes?feature=oembed&w=500&h=281]

Modified Version:

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=a-OJlwb4k6s?feature=oembed&w=500&h=281]




40 AMENIWEKA huru kweli

40

1. Ameniwaka huru kweli, naimba sasa: Haleluya! Kwa msalaba nimepata kutoka katika utumwa.

Pambio:
Nimeokoka, nafurahi! Na dhambi zangu zimetoka. Nataka kumtumikia Mwokozi wangu siku zote.

 

2. Zamani nilifungwa sana kwa minyororo ya shetani, nikamwendea Bwana Yesu, akaniweka huru kweli.

 

3. Neema kubwa nilipata kuacha njia ya mauti, na nguvu ya wokovu huo yanichukua siku zote.

 

4. Na siku moja nitafika mbinguni kwake Mungu wangu. Milele nitamhimidi na kumwimbia kwa shukrani.

 

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=1s24X-6Hv2k?feature=oembed&w=500&h=375]

 




41 SIKU nyingi nilifanya dhambi

41

1. Siku nyingi nilifanya dhambi, sikujua Neno la Mwokozi, sikujua maumivu yake kwa ‘jili yangu.

Pambio:
Bwana Yesu alinirehemu, dhambi zangu alizichukua. Namsifu Yesu kwa ajili ya msalaba.

2. Niliposikia Neno lake, moyo wangu ukalia sana. Nikaona maumivu yake kwa ‘jili yangu.

3. Bwana Yesu ni Mwokozi wangu, jua na Mfalme na uzima. Ninamhibidi kwa ajili ya msalaba.

William R. Newell, 1868-1956
Years I spent, R.S. 773




42 BWANA Yesu amevunja minyororo ya maovu

42

1. Siku nyingi nilifanya dhambi, sikujua Neno la Mwokozi, sikujua maumivu yake kwa ‘jili yangu.

Pambio:
Bwana Yesu alinirehemu, dhambi zangu alizichukua. Namsifu Yesu kwa ajili ya msalaba.

 

2. Niliposikia Neno lake, moyo wangu ukalia sana. Nikaona maumivu yake kwa ‘jili yangu.

 

3. Bwana Yesu ni Mwokozi wangu, jua na Mfalme na uzima. Ninamhibidi kwa ajili ya msalaba. William R. Newell, 1868-1956




117 NILIPOFIKA Golgotha

117

1. Nilipofika Golgotha nikaiona huko neema kubwa kama mto, neema ya ajabu.

Pambio:
Neema ya Golgotha ni kama bahari kubwa, ne’ma tele na ya milele, ne’ma ya kutosha!

 

2.Nilipofika moyo wangu ulilemewa sana, sikufaamu bado vema neema yake kubwa.

 

3.Nilipoona kwamba Yesu alichukua dhambi, neema ikadhihirika, na moyo ukapona.

 

4. Mbinguni nitakapofika, furaha itakuwa kuimba juu ya neema milele na milele.

E.O. Excell, 1905

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=LzmnlJlVZFc?feature=oembed&w=500&h=281]




127 NIMEUONA mto safi

 127

1. Nimeuona mto safi, kisima cha ajabu, ni damu yake Yesu Kristo, inayonitakasa.

Pambio:
Nimeuona mto safi uniosha moyo wangu. Namshukuru Mungu wangu, aliniweka huru kweli!

 

2. Kwa nia na dhamiri safi naendelea mbele, ninasafiri kwenda mbingu kuona raha yake.

 

3.Neema kubwa, nimeonja uheri mbinguni, maana damu yake Yesu imeniponya moyo!

 

Mrs. Pheber Palmer
The cleansing bood, Sgt. 18. MA.




142 KWANAMNA nyingi nilitafuta kupata raha moyoni mwangu

1. Kwa namna nyingi nilitafuta kupata raha moyoni mwangu. Unyonge wangu haukukoma ila kwa Bwana Yesu.

 

2. Na moyo wenye hatia nyingi nilimwendea Mwokozi wangu, na alinipa wokovu wake na nguvu ya kushinda.

 

3. Kwa pendo kubwa Mwokozi wangu aliuweka uzima wake, si kitu mimi ulimwenguni, nina wokovu kwake.

 

4. Ijapo ninachukiwa huku ni mteule wa Bwana Yesu, napenda sasa kumfuata, nifike kwake Mungu!

 




144 SAWA na kisima safi

1.Sawa na kisima safi, chenye maji mengi, mema, ni upendo wa Mwokozi ukaao ndani yake.

Pambio:
Yesu amelifungua lango zuri la mbinguni ili niingie humo kwa neema yake kuu.

2. Kama ndege awindavyo mara nyingi niliumwa, Moyo wangu ulilia, Yesu hakunifukuza.

3.Ni ajabu kubwa kweli, alinisamehe yote! Juu ya rehema yake ninaimba kwa furaha.

4.Asubuhi ya uzima nitafika mlangoni; kwa ajili ya upendo nitapata kuingia.

Fredrick Bloom, 1917




149 UZIMA ninao moyoni daima

1. Uzima ninao moyoni daima, uzima ni Yesu Mwokozi, aliyeingia rohoni hakika, akanitilia ‘hodari.

Pambio:
Nashiba rohoni kwa raha ya Mungu, na moto wa mbingu ulimo. Napata kukaa nuruni kabisa, na nuru ni Yesu Mwokozi.

2. Baraka zilizo katika wokovu nilizozipata kwa bure, nilipoungama makosa na dhambi kwa Yesu Mwokozi wa wote.

3. Mwokozi aliniondoa porini, natunzwa shambani mwa Mungu. Na sasa kwa mvua na jua la mbingu ninamzalia matunda.

4. Naona maisha ni yenye maana: Ni ku’tumikia Mwokozi. Kuishi ni Kristo na kufa faida kwa kila mkristo wa kweli.


Video ya sauti

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=u44R7u9d8aE?feature=oembed&w=500&h=281]




189 UNIHUBIRI habari njema

189

1.Unihubiri habari njema, neno la ukombozi, hata ikiwa siufahamu wingi wa wema! Nilipokuwa katika giza, ndipo Mwokozi alinijia, na akanipa wokovu, raha na tumaini.

Pambio:
Mimi kipofu, naona sasa, anasikia maombi yangu, naye hatanisahau, kwani ananipenda.

 

2. Amefungua mkono wake, kuna wokovu humo; ukilemewa moyoni mwako, uje kwake Yesu! Uliyechoka kwa dhambi zako, umtazame Mwokozi wako, na utapata wokovu, njoo, anakupenda.




197 HAPO nilipokua dhambini

197

1. Hapo nilipokuwa dhambini, niliumwa kwatika roho. Sasa ninafurahi kwa shangwe kwani Yesu ameniponya.

Pambio:
Ndiyo kazi kubwa ya ajabu: Mwokozi aliniokoa! Naye anapenda watu wote, atakuokoa wewe.

 

2. Dhambi zote nilizozitenda zimefutwa na Bwana Yesu. Sikitiko kwa ‘jili ya dhambi zilikoma nilipotubu.

 

3. Sasa mimi sitaki kurudi, nachukia kabisa dhambi. Nimeonja furaha ya Mungu na amani na raha yake.

T. Allan Törnberg




230 GOLGOTHA Mwokozi alitundikwa mtini

230

1. Golgotha Mwokozi alitundikwa mtini kwa’jili ya wote. Na damu akaitoa Mwokozi ili kutangua dhambi.

Penye msalaba nilikombolewa kwa damu ya Yesu iliyotolewa. Mwamuzi mwenyewe alinikomboa, akanilipia deni.

 

2. Golgotha nami nimesulibiwa pamoja na Yesu Mwokozi; na njia kwa Mungu Baba ni wazi, pazia limepasuka.

Nimesulibiwa pamoja na Kristo, na mtu wa kale alikufa hapo. Na mambo ya kale yamekwisha’pita, lo! yote ni mapya sasa!

 

3. Niliunganishwa naye Mwokozi, na sasa ni hai kwa Mungu. Kuishi ni Kristo, siri ajabu, na kufa faida kwangu!

Kwa damu ya Yesu nimetakasika, hatia na dhambi zimeondolewa. Shetani hawezi kunidhuru tena, nimewekwa huru kweli.

Henrik Schlager, 1870-1934




232 NILIPOFIKA kwa bwana Yesu

 232

1. Nilipofika kwa Bwana Yesu, nikapaaza sauti yangu: “Yesu Mwokozi, unirehemu!” Akaniokoa.

:/: Yesu asifiwe! :/: Alisikia kilio changu, Yesu asifiwe!

 

2. Nilipofika kwa Bwana Yesu, nikamsihi Mwokozi wangu: “Unitakase, nifanye safi!” Akanisikia.

:/: Yesu asifiwe.:/: Alisikia maombi yangu, Yesu asifiwe!

 

3. Ona kisima cha msalaba, leo kingali chabubujika kuniokoa na kusafisha! Yesu asifiwe!

:/: Yesu asifiwe:/: Aniokoa, anisafisha, Yesu asifiwe!

 

4. Njoo kwa Yesu, kisima hicho, unywe, uoshwe katika maji! Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe.

:/: Yesu asifiwe! :/: Kiu yapoa, na watakaswa, Yesu asifiwe!

E.A. Hoffman, 1877
Down at the Cross, R.S. 192




235 TUMEKOMBOZWA katika nchi

1. Tumekombozwa katika nchi, usikilize vema, rafiki!
:/: Tumeokoka tufike juu, taji kutiwa, furaha kuu! :/:

 

2. Tumekombozwa katika watu, hata tuchekwe kitambo huku.
:/: Twavumilia katika shida, twatazamia ‘heri wa mbingu. :/:

 

3. Tumekombozwa, tuwe wa huru, tukichokozwa haitudhuru.
:/:Tutaondoka, ‘hamia mbingu, tutasimama mbele ya Mungu.:/:

 

4. Tumekombozwa, furaha kuu, twaandaliwa karamu kuu!
:/: Salamu hiyo uitangaze, wafike mbio na waokoke! :/:

 

5. E’ mama, baba, mbona kungoja? Ndugu na dada, fika pamoja!
:/: Mwenye kukawa hataingia, leo waitwa na Yesu pia. :/: R.

Edhelgerg




236 DHAIFU mwenye dhambi

236

1. Dhaifu, mwenye dhambi, nilipotea njia, lakini Bwana Yesu alinihurumia. Nategemea yeye, najua pendo lake, ajaza roho yangu, ninavyo vyote mwake.

Pamio:
Ajaza roho yangu, apita vitu vyote. Amani na upendo ni zangu siku zote. Ajaza roho yangu, neema kubwa kwangu! Namhimidi Yesu: Yu yote ndani yangu.

 

2. Sitaki dhambi tena, haiku’faidia; rafiki yangu, Yesu, ananisaidia. Alitangua dhambi kwa msalaba wake, kwa yeye ukombozi, na vyote vimo mwake.

 

3. Napenda kufuata daima nyayo zake, nibadilishwe sana, nifananishwe naye! Na tena siku moja atanikaribisha nyumbani mwake Baba, na atanijaliza!

Otto Witt




250 IKAWA siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu

 250

1. Ikawa siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu. E’ roho yangu umsifu Mwokozi wako Yesu Kristo!

Pambio:
Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu! Na kwa neema na upendo akaondoa dhambi zangu! Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu!  

 

2.Nimeokoka, nafurahi! Ananitaja mwana wake! Alinivuta kwa upendo, nikafuata mwito wake.

 

3.Ni shangwe ku’ moyoni mwangu nikifuata Bwana Yesu. Anipimia ne’ma sawa wakati wote ma maisha.

 

4. Kwa pendo kubwa na rehema ananitunza siku zote. Sitasaahu siku ile aliyoniokoa Yesu.

Oh, happy day, R.Sl 622; R.H. 619




251 HERI mimi kwani Mukombozi wangu alitoa dhambi

251

1. Heri mimi kwani Mkombozi wangu alitoa dhambi zote! Shangwe na furaha zanijaza mno, kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi!

Kila siku nafurahi! Heri mimi kwani Mkombozi wangu alitoa dhambi zote!

 

2.Heri mimi, Yesu alinifilia; ni furaha ku’; yu hai! Ni rafiki kweli anayetuweka huru toka minyororo.

Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi Yesu alinifilia; ni furaha ku’: Yu hai!

 

3.Heri mimi kwani ananiongoza; nafuata nyayo zake. Nikiyasikia tu maneno yake, sitaweza kupotea.

Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi kwani ananiongoza, sitaweza kupotea!




281. YOTE ninayo niliyapokea kwa wema wake

 281

1. Yote ninayo niliyapokea kwa wema wake unaonea. Namsifu Yesu, namtegemea, aliniokoa kwa neema.

Pambio:
Niliyekuwa nimetoroka, kwa pendo lake nimeokoka. Yesu yu mwema na mwenye rehema, nimeokolewa kwa neema!

 

2. Nilitembea zamani dhambini katika njia ya kufa, lakini Yesu alinitafuta porini, akaniokoa kwa neema.

 

3. Natakasiwa na Yesu Mwokozi, si kwa majuto na si kwa machozi, bali kwa damu, ninao ‘kombozi; nimeokolewa kwa neema.

 

4. Raha ya mbingu imeniingia, kwa shangwe kubwa ninafurahia Yesu, kwa kuwa anirehemia; nimeokolewa kwa neema.

J.M. Gray, 1905 Otto Witt, 1922
Naught have I gotten, RS. 605




296. Dhambi hatia zimeondolewa

296

1. Dhambi, hatia zimeondolewa, yote ya kale yamepita sasa. Damu ya Yesu imenisafisha; ninamfurahia Mkombozi wangu.

Pambio
Mavazi safi na kao nzuri ninayo huko ju’ mbinguni. Thawabu nita’pewa huko ni taji ya uzima. Na Yesu ni Mwokozi wangu. Alinikomboa, alilipa deni langu. Pendo lake kubwa nina’sifu siku zote, ninamfurahia Mkombozi.

 

2. Siku za manung’uniko zimekwisha, nimeokoka katika utumwa. Sasa naona raha na furaha sababu Bwana Yesu alinikomboa.

 

3. Shaka na hofu zimeondolewa, na siogopi kufa kwangu tena. Katika Yesu ninatumaini. Na ninalindwa vema naye siku zote.

 

4. Roho wa Mungu amenijaliza, anifariji katika mwenendo. Yesu Mwokozi yu karibu nami, aliye ngao yangu na makimbilio.