116 TUIMBIE tumsifu Yesu ju’

116

1. Tuimbie, tumsifu Yesu ju’ya msalaba! Aliteswa na akafa, yote kwa ajili yetu. Akashinda, ‘kafufuka, ni Mwokozi ‘kamilifu.

Pambio:
Yesu alitukomboa, na akawa haki yetu. Dhambi aliziondoa, akatupa tumaini: Tutarithi utukufu, nuru, raha na uheri.

 

2. Yesu alipofufuka akatushindia kufa, akapewa nguvu zote duniani na mbinguni. Sisi sote tumepona kwa kupigwa kwake Yesu.

 

3. Tushukuru Mungu Baba kwa ajili ya upendo! Tumsifu Yesu Kristo kwa neema yake kubwa! Tumfungulie moyo kwake Roho ‘takatifu!

 

Venatius Fortanus, env. 600




152 YESU alipolala kati’ kaburi

152

1. Yesu alipolala kati’ kaburi, giza ilifunika Yesu Mwokozi.

Pambio:
Alifufuka hakika, akavunja nguvu ya mauti, mshindaji ju’ ya mamlaka yote; ni Mflme wa milele na milele, Alikuwa amekufa, na tazama amefufuka!

 

2. Walinzi wa kaburi walikimbia, muhuri na vifungo vilivunjika.

 

3. Mauti na pingo hazikuweza kumshika Yesu Mwokozi.




153 YESU CHRISTO alifufuka

153

1. Yesu Kristo alifufuka, akatoka kaburini. Furahini na msifuni, kwani alishinda kufa!

Pambio:
Habari njema: Alifufuka katika wafu! Yesu yu hai, naye atakuja tena.

 

2. Nguvu za mauti na dhambi Yesu Kristo alishinda; nasi sote tutashinda kwa nguvu yake ya ajabu.

 

3. Kundi dogo, msiogope, Bwana Yesu ni uzima! Aliziondoa dhambi na anawafariji moyo.

 

4. E’ wakristo, shangilieni, Yesu aliyefufuka yu karibu, atakuja na atatufufua sote!

Eric Bergqvist, 1904




284. USIMTAFUTE Yesu kati’wafu kaburini

284

1. Usimtafute Yesu kati’ wafu kaburini! Yu mzima, tumsifu, hakushindwa na kuzimu!
:/: Yesu hai, Yesu hai, mshindaji wa mauti! :/:

 

2. Maadui walifunga Bwana Yesu kaburini, Mungu alimfufua Mwana wake. Furahini!
:/: Yesu hai, Yesu hai, imba hivyo duniani! :/:

 

3. Yesu hai, ni habari ya kupasha pande zote. Yu Mwokozi wetu kweli, alitufilia sote.
:/: Yesu hai, Yesu hai, Mkombozi asifiwe!:/:

P.P. Bliss