217 BWANA Yesu atakuja kutoka mbinguni

217

1. Bwana Yesu atakuja kotoka mbinguni, atawachukua wote wanaomwamini.

Pambio:
Kama nyota za mbinguni watu wake watang’aa katika taji yake, kuwa sifa ya Yesu.

 

2. Atawakusanya wote waliompenda, watakuwa tunu yake milele mbinguni.

 

3. Na watoto watakuwa pamoja na Yesu, watang’aa kama lulu nyumbani mwa Baba.

G.F. Root




218 MTOTO mimi ni maskini

218

1. Mtoto mimi ni maskini, lakini nafurahi kwa kuwa Baba yangu mwema ananitunza vema.

 

2. Babangu anipenda sana, anionyesha njia. Upendo wake unapita uzuri wa dunia.

 

3. Katika shida na huzuni naimba kwa furaha: “Nina makimbilio yangu kwa Mungu Baba yangu”.




221 E’MTOTO yainue macho yako mbinguni

221

1. E’mtoto, yainue macho yako mbinguni! Bwana Yesu huko juu, kwa upendo akuone.

 

2.Ukiomba asikia, akulinda mashakani; na anakuandalia kao zuri huko kwake.

 

3. Penda Yesu, mfuate, tii neno lake pia! Tena malaika wake watakuchukua kwake.




223 NI UHERI bora kumwamini

 223

1. Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu, kabla hatujazionja dhambi na mashaka zinazoharibu roho zetu.

Pambio:
Ni uheri bora kumwamini Bwana Yesu, na kumfuata kila siku. Na ujana wetu ukitukimbia tena, shangwe ya wokovu itabaki.

 

2.Ni uheri bora kumtii Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Hivyo tutakuwa na dhamiri safi, njema kwa maisha yetu yote pia.

 

3.Ni uheri bora kumtumikia Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Bwana Yesu akumbuka kila tendo dogo, atalipa kwa neema yake.

 

4.Ni uheri bora kumngoja Bwana Yesu kwa wakati wa ujana wetu. Atatuchukua kwake kwa furaha kubwa, tutakuwa naye siku zote.




225 LO! bendera mbele yako

225

1. Lo! Bendera mbele yako, usihofu sasa! Usimame kwa imara kama Danieli!

Pambio:
Uwe mhodari kama Danieli! Weka makusudi mema bila kuogopa!

 

2. Wenye hofu hawawezi kuingia mbingu. Tweka tu bendera yetu, endelea mbele!

 

3. Mashujaa wa shetani wangeshindwa sana wakikuta jeshi la askari wa imani.

 

4. Endelea kwa kushinda, Yesu ni Mfalme! Taji ya uzima utapata huko juu.




226 MACHO yangu ya kumtazama

226

1. Macho yangu kumtazama, masikio yakumsikia, na miguu yakumfuata Yesu, rafiki yangu!

 

2. Roho yangu inapenda Yesu, na ulimi unamshukuru, kwa mikono namtumikia Yesu, rafiki yangu!




227 MUNGU aliye mbinguni alitupa kiongozi

227

1. Mungu aliye mbinguni alitupa kiongozi, naye ni rafiki wa watoto wote. Ukijua jina lake, ulitaje sasa hivi! Anapenda wote, hata wewe, nami.

Pambio:
Mbingu na ufalme wake wa wototo wote sasa! Mbio tuishike njia iendayo kwake Yesu ili tuione raha ya mbinguni!

 

2. Yesu mwenye pendo kubwa awakumbatia wote, anawabariki kwa huruma yake. Hatuoni huku chini mtu mwema kama yeye, hasahau mtu, hata mnyang’angyi.

 

3. Yesu ni Mchunga mwema, anawakusanya sasa mkononi mwake wana wa kondoo. Kifuani mwake tena anawachukua wote hata kwa ufalme wake huko juu.