16 YO YOTE uonayo huku katika mwendo wako

16

1. YO yote uonayo huku katika mwendo wako, Yafaa kumwambiya Yesu atakusaidia.

Refrain:
:/: Kwa kuwa kila aombaye Mwokozi ne’ma yake, ataokoka na hatia, na atasifu Yesu. :/:

2. Ukichukiwa na wenzake na ukijaribiwa, Mwokozi yu karibu sana, Maombi asikia.

3. Ukiwa mwana mpotevu, na mbali na Babako, Amani una’kosa sasa, Urudi kwake Yesu!

4. Ukiwa na makosa mengi, Na roho yako ngumu, Neema yake yakutosha, utubu dhambi zako

5. Ikiwa nguvu mara nyingi kuomba kwa bidii, uombe Baba, kama mwana, akusikia kweli!

Carl Lundgren


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=ZR8mfMstQws?feature=oembed&w=500&h=281]




28 NINATAKA kufuata wewe

 28

1. Ninataka kufuata wewe, Yesu, siku zote, ‘kiwa katika furaha au shida na udhia. Unaponitangulia ninakuja nyuma mbio. Ninajua ni karibu Kuwasili huko kwako.

 

2. Haifai niulize: Bwana, unakwenda wapi? Au kwa kusitasita kuishika njia yako. Kweli hapa kazi moja: Kufuata wewe mbio, kwenda njia ile moja wewe unionyeshayo.

 

3. Walakini kama kitu kinataka kunifunga, au kuwa mgogoro katita safari yangu, ‘kate kamba mara moja ifungayo roho yangu! Ninataka kuwa huru kukutumikia vema

 

4. Bwana Yesu, unilinde, uhifadhi nia yangu! Nikichoka kwa safari, nong’oneza kwa upendo: «Mwana, u mtoto wangu, uniandamie punde, utapumzika sana tena kwangu huko juu».

 

Lina Sandell-Berg, 1896
o Jesus, Sgt. 605 (231)




29 UNIVUTE Yesu

29
1. Univute, Yesu, nifuate nyayo zako, ‘kiwa kwa rafiki au katika wageni, na mahali pa furaha au sikitiko; sina budi kumkaribia Yesu.

Pambio:
Nimfuate, nimkaribie, siku zote na popote nimwandame Yesu! Nimfuate, nimkaribie, Yesu mbele, nami nyuma, hata mwisho!

2. Juu ya milima nitasikiliza Yesu, hata mabondeni nitaandamana naye. Jua, giza, afya, ‘gonjwa, utulivu, vita, kati’ hayo yote Yesu yu karibu.

3. Nikiteka maji, au nikilima shamba, nikika’ nyumbani au ‘kiwa safarini, hata huko soko neno moja ni halisi: Sina budi kumkaribia Yesu

Down in the valley, R.H. 245




31 KATIKA safari yetu kwenda huko juu tusilale usingizi

31

1. Katika safari yetu kwenda huko juu tusilale usingizi, tuwe na bidii!

Pambio:
Kaza mwendo tusifungwe, twende mbio tu! Yesu Kristo ni Mwokozi na Mfalme ‘kuu!

 

2. Bwana Yesu anatupa maji ya uzima, maji hai ya milele ya kuburudisha.

 

3. Njia na miiba mingi inatuzuia, hofu na hatari nyingi zina fadhaisha.

 

4. Mungu wetu atungoja huko kwake juu, Yesu ni Mwokozi wetu, tufuate Yeye!

P.P. Bliss




33 HURU kama ndege bustanini

33

1. Huru kama ndege bustanini, sasa nafurahi kwa sababu Yesu ni rafiki yangu ‘kubwa; nina amani siku zote.


2. Aliniokoa na mashaka, alinipa tunu ya rehema. Mimi ni mtoto wa babangu, na nuru inang’aa sana.


3. Ninataka ku’shukuru Bwana, alitupa dhambi zangu mbali, na sitaziona tena kamwe, hazitanitawala tena.


4. Jua likifichwa kwa mawingu, kiti cha rehema ni karibu, hayo ndipo shida ziishapo, na roho yangu yatulia.


5. Radhi kama mwana kwa babake, kwa salama kama bandarini, Ninapumzika kwa Mwokozi, mbali na shida na huzuni.


6. Yesu yu karibu siku zote, achukua mimi na mzigo. Napokea kwa mkono wake neema na mateso pia.


7. Nilimpa Yesu moyo wangu, ninapenda kumtumikia; neno lake linapendwa nami, na nira yake ni laini.


8.Nafurahi sana kanisani kati ya watoto wa babangu, Roho ya neema ni karibu, kunanifurahisha sana.


9. Mimi ni mdogo duniani, tena msafiri na mgeni. Kwetu ni mbinguni huko juu; babangu ananiongoza.


10. Saa za mashaka zitakwisha, kuja kwake Yesu ni karibu. Nitaona raha kubwa sana katika nyumba ya babangu.

Nils Frykman




35 NIMEFIKA kwake Yesu

35

1. Nimefika kwake Yesu, Na rohoni mwangu sasa, jua lake la neema linang’aa kila siku.

Pambio:
Roho yangu inaimba, nimefunguliwa kweli. Nimekaribia Yesu, ninaimba kwa furaha.

2. Pepo za neema yake zinavuma ndani yangu, na mawimbi ya wokovu yananijaliza sasa.

3. Sasa Bwana Yesu Kristo amefanya kao kwangu. Nimepewa mfariji, Roho ya ahadi yake.

4. «Siku roho afikapo mtajua kwa hakika kwamba ninakaa kwenu», hivyo Yesu alisema.

5. Kweli, amefika kwetu, sasa yumo ndani yetu. Ujitoe kwake Mungu, aioshe roho yako!

6. Yesu atakapokuja katita utakatifu, nitafananishwa naye, nitamshukuru sana.

Pambio:
Zitakuwa nyimbo nyingi tuta’poingia mbingu, na milele tutaimba na kusifu Mungu wetu.

Werner Skibsted




39 YESU ameingia katika roho yangu

39

1. Yesu ameingia katika roho yangu, amenifungulia kamba za dhambi zangu. Tena amenijaza Roho Mtakatifu. Ninamsifu sasa kwa wimbo mpya.

Pambio:
Yesu ni yote kwangu, yote na’pata kwake. Ameondoa dhambi, ametakasa mimi. Shangwe rohoni mwangu ni kama maji mengi, namshukuru sana Mwokozi wangu.

2. Siku si ndefu tena, kazi si ngumu sasa, njia yanipendeza, ‘kiwa nyembamba sana. Katika hali zote ninamwimbia Yesu, yeye Mfalme wangu, ninamsifu!

3. Katika mwendo wangu ninazidishwa shangwe, hata wakinicheka, mwovu akijaribu. Hima Mwokozi wangu atanyakua mimi toka machoni pao. Haleluya!

Ivar Lindestad




44 Tu watu huru

44

1. Tu watu huru, huru kweli katika Yesu Kristo. Tunahubiri neno lake kwa moto ‘takatifu. Tuendelee, mbele, mbele, tukashinde majaribu! Twapiga vita ya imani, tuvumilie yote!

 

2. Tu jeshi kubwa la askari, tu safi kati’ damu. Mfalme wetu, Yesu Kristo, ni kiongozi wetu. Kwa nguvu yake kubwa mno tutadumu hata kufa.Tuendelee, mbele, mbele, tumshukuru Mungu.

 

3. Kwa Yesu tuna uhodari na mamlaka kubwa, maana tunayaamini maneno yake yote. Kisima wazi, cha ajabu, kinatoka msalaba, tuliyakunywa maji yake, ni maji ya uzima.

 

4. Mbinguni nchi ya asili [raha], ya haki na amani, tuta’pofika huko juu tutamwimbia Yesu. Na kila chozi litafutwa na mkono wa Mwokozi. Kwa shangwe kubwa tutarithi ufalme wa ahadi.

Werner Skibsted




45 WAIZRAELI walika’ Babeli utumwani

45

1. Waisraeli walika’ Babeli utumwani, wakawa na huzuni tu kwa ‘jili ya sayuni.

Pambio
Hapo amri ilifika waliweza kuondoka, shangwe gani mioyoni mwao! Walitwaa vinubi vyao, wakaenda wanaimba hadi, hata kurithi nchi yao.

 

2. Vinubi havikubigwa wakati wa utumwa, na walikaa kimya tu mahali pa ugeni.

 

3. Walipotoka Babeli, ikawa kama ndoto; furaha nyingi rohoni, faraja na uheri.

 

4. Mataifa walisema: «Mungu umefanyaje? Watumwa wameondoka, wamewekwa huru»!

 

5. Katika ulimwengu hu’ ni wengi wafungwao. Uhuru ni kwa Yesu tu kwa kila a’miniye.

Pambio:
Ndiye ameleta amri: Tunaweza kuokoka, shangwe ku’kwa kila ‘aminiye! Njoo sasa, twa’ kinubi, tufuate kwa kuimba hata kuirithi nchi yetu!

Werner Skibstedt




47 NIKIONA udhaifu na imani haba

47

1. Nikiona udhaifu na imani haba, nikijaribiwa sana, Yesu anilinda.

Pambio:
Anilinda vema, anilinda vema, kwani Yesu anipenda, anilinda vema.

 

2. Peke yangu sitaweza kuambata yeye, pendo langu ni dhaifu; Yesu anilinda.

 

3. Mimi mali yake sasa, alinikomboa, alitoa damu yake; Yesu anilinda.

 

4.Haniachi kupotea, anilinda sana. Kila ‘mwaminiye kweli, Yesu amlinda 

R. Habershon




49 NJIA yote naongozwa kwa mkono wa Mwokozi

 49

1. Njia yote naongozwa kwa mkono wa Mwokozi, ninapo wema wake, sina shaka, hofu tena. Nina raha ya mbinguni, ninakaa kwa salama. :/: Na katika mambo yote ananitendea mema. :/:

2. Njia yote naongozwa, namtegemea Yesu. Anilinda jaribuni, anitia nguvu pia. Nikiona kiu hapa, nikichoka safarini,:/: Mwamba uliopoasuka unabubujika maji. :/:

3. Njia yote naongozwa kwa mkono wake bora, atanituliza tena kwa babake huko juu. Miguuni pake Yesu ninataka kusujudu,:/: Nakusifu yeye, kwani aliniongoza huku. :/:

Fanny Crosby, R. Lowry, 1875
All the way my Saviour leads me, R.S. 445




51 NAONA amani Golghota alipo jitoa Mwokozi

51

1. Naona amani Golgotha alipojitoa Mwokozi,
:/:Na huko nina kimbilio kwa Yesu aliyejitoa.:/:

 

2. Sitaki ‘tamani fahari na dhambi katika dunia,
:/: Sababu wokovu ninao katika ‘jeraha ya Yesu. :/:

 

3. Aliziondoa kabisa mizigo na kamba ya dhambi.
:/: Na niliokoka halisi kwa neno la Mungu wa ‘hai. :/:

 

4. Maneno ya Mungu ni kwetu chakula na dawa ya roho,
:/: na nguvu ya kusaidia mkristo katika safari. :/:

 

5. Mimi sasa hekalu la Roho, anayemiliki moyoni;
:/: na Yesu ataniongoza kwa njia ya ahadi zake. :/:

 

6.Uliye dhambini ufike kwa Yesu Mwokozi wa wote!
:/: Anakunyoshea mikono ya pendo kukusaidia. :/:




58 UNIPE raha tele kama mto

58

1. Unipe raha tele kama mto, nipite jangwa huku kwa furaha; unipe imani tena, Yesu, ningoje siku yako kwa bidii!

 

2. Kwa siku chache ninaona shida, dhoruba zinanisumbua huku. Napanda mbegu zangu nikilia, lakini nitavuna kwa furaha.

 

3. Kwa siku chache ninaburudishwa mtoni penye njia yangu huku, lakini siku kubwa itafika, nita’inywea chemchemi yake.

 

4. Kwa siku chache naitunza taa, nadumu kwa kuomba na kungoja. Na siku za uchungu ziishapo, nitamkuta Yesu huko juu.

Jane Crewdson




67 TUNAKARIBIA kao la mbinguni

67

1. Tunakaribia kao la mbinguni, hata jua likifichwa na mawingu. Tufuate Bwana Yesu siku zote, ni furaha yetu kumwandama yeye!

Pambio:
Tunakaribia mbingu kati’ yote, haleluya! ‘sifuni Mungu! Jipe moyo safarini kwani Yesu yu pamoja nasi hata mwisho!

 

2. Tunakaribia kao la mbinguni, hata tukiona pepo na dhoruba. Bwana yu karibu, na uwezo wake ni makimbilio yetu hatarini.

 

3.Njia yetu inapita kati’ jangwa, na miguu inauma mara nyingi, walakini tunakwenda tukiimba na kusifu Yesu, Mwokozi wetu.

 

4. Mwendo wetu utaisha siku moja, tutapata kustarehe huko juu. Tukiona shaka, shida hapa chini, tutapata utulivu kwake Yesu.

Pambio:
Tunakaribia mbingu kati’ yote, haleluya! ‘sifuni Mungu! Tunataka kufuata hata mwisho. E’ rafiki, utuandamie!

Nathan Cronsie, 1914




71 NIMEKWISHA kuingia nchi nzuri ya ahadi

71

1.Nimekwisha kuingia nchi nzuri ya ahadi, nchi njema ya wokovu wake Mungu. Huko ni vijito vingi vya baraka na furaha, huko shida haifiki.

Pambio:
Nimekwisha kuingia nchi nzuri ya ahadi. Moyo wangu hufurahi, ninaishi kwa neema.

 

2.Nimefika kanaani, hapo ni urithi wangu, na sitaki kuondoka tena kamwe. Sasa nira ni laini na mzigo si mzito, Yesu ni furaha yangu.

 

3.Nimekwisha kuingia nchi ya amani kuu, hata mwili wangu unatiwa nguvu. Nchi hiyo ni ya raha na faraja imo pia, hapo tunaka’ salama.

 

4.Nime’ngia nchi hiyo, ndiye Bwana Yesu Kristo, ninakaa tatika urithi wangu. Kwa imani ninakunywa maji hai ya kisima, huku ni furaha kubwa.

 

5.Nitafika hata mbingu, nchi ya hazina yangu, dhambi na mateso hazitakuwako, wala giza ya usiku, wala sikitiko chungu, wala shida, wala kufa. Werner Skibsted




72 MIMI mgeni katika dunia

72

1. Mimi ngeni katika dunia, ninasafiri kufika mbinguni. Hata ikiwa hatari njiani, nitaishinda pamoja na Mungu. Kama Ibrahimu majaribuni nita’vyoshinda kwa nguvu ya Mungu. Nitavumilia nifike mbinguni, ndilo kusudi la moyo.

 

2.Nikitembea gizani kabisa mimi mnyonge pamoja na Yesu, na nikipita motoni, majini, nakusudia kufika mbinguni. Mungu ajua mapito jangwani, naye Mwenyezi atanifikisha. Nitavumilia nifike mbinguni, ndilo kusudi la moyo.

 

3. Tusisumbuke katika safari, tuwatazame wali’tangulia! Yesu Mwokozi alitukomboa, msalabani alitufilia! Naye atatufikisha mbinguni; hivi tuimbe kwa mda kitambo: tutavumilia tufike mbinguni, ndilo kusudi la moyo!




76 MGENI mimi

76

1. Mgeni mimi, ninasafiri siku chache, siku chache huku chini. Msinipinge, niwafuate watakatifu walioshinda! Mgeni mimi, ninasafiri siku chache, siku chache huku chini.

 

2. Nashika njia, napiga mbio, sina budi kuukuza mwendo wangu. Na kwa mkono natwaa gongo, nazo silaha nimejivika. Nashika njia, napiga mbio, sina budi kuukuza mwendo wangu.

 

3. Ulimwenguni sipati raha, natamani ku’fikia mji mpya. Machozi, kufa, maombolezo sitayaona mbinguni tena. Ulimwenguni sipati raha, natamani ku’fikia mji mpya.

 

4. Mchunga mwema, ninakuomba, ‘tangulie, niongoze njia yote, kwa kuwa giza na dhambi tena zaniwekea mitego mingi! Mchunga mwema, ninakuomba, ‘tangulie, niongoze njia yote!




79 MAISHA mafupi yahuku dunia

79

1. Maisha ya mtu [mafupi] ya hapa dunia yanaifanana safari chomboni. Twapita bahari katika hatari, lakini Mwokozi anatuongoza.

Pambio:
Ikiwa Mwokozi anatuongoza twaweza kuona amani na raha, atatufikisha salama mbinguni, na humo hatutakumbuka safari.

 

2. Twapita katika baridi na pepo, maneno ya Mungu ni nuri gizani. Hatari na hofu na chombo kibaya hatuta’kumbuka karibu na Yesu.

 

3.Ingawa mawimbi yapiga kwa nguvu, tunakaribia bandari upesi. Na humo hakuna dhoruba na pepo; safari tutaimaliza salama.

 

4. Tutakapofika bandari ya mbingu tutamshukuru Mwokozi mkuu. Hatutaziona hatari na hofu karibu na Yesu mwenyewe mbinguni.




81 ALIPOKUFA Yesu ju’ ya musalaba

81

1. Alipokufa Yesu ju’ ya msalaba wake akaishinda dhambi na uwezo wa shetani. Aliniweka huru, niwe mbali na hatia; na tena atanichukua kwake.

Pambio:
Mbinguni niendako haitakuwa dhambi, ni nchi nzuri ya salama mno. Na Bwana, Mungu wetu, atatuangazia; tukusanyane sisi sote humo!

 

2.Ninafuata njia ya Mwokozi wangu sasa, aniongoza vema, anafuta kila chozi. Ananilinda katika hatari za njiani, karibu naye vita yatulia.

 

3. Mbinguni nchi yangu, na bendera ni upendo, na Roho arabuni ya urithi wangu huko; na neno lake ni chakula changu safarini; neema inanipeleka kwake.

Carl Widmark, 1912




139 NINAFURAHA kubwa

1. Nina furaha kubwa, napumzika sana, kwa kuwa nimefika kwa Mungu, Baba yangu. Ameniweka huru na mbali na utumwa, na sasa nakaa salama.

 

2. Zamani nilidhani kuacha dhambi zote, lakini sikuweza kushinda peke yangu. Ninamwamini sasa Mwokozi wangu, Yesu, na yeye ananishindia.

 

3. Mwokozi wangu, Yesu, aliyenifilia, aliokoa mimi, angali anipenda; nahesabiwa haki katika damu yake, inayosafisha kabisa.

 

4. Na nikijaribiwa na mwili wangu tena, ninakumbuka Yesu, apita vitu vyote. Neema yake kubwa kuliko dhambi zangu. Ninamshukuru Mwokozi.

 

5. Na sasa Bwana Yesu akaa ndani yangu, neema yake kubwa yanizunguuka mimi. Sitasumbuka tena, nimejiweka kwake, na Mungu anilinda vema

 

6. Shetani akitaka kufanya vita sasa, sitaogopa yeye na mamlaka yake. Maneno yake Mungu, ni yenye nguvu sana kwa wote wanaoamini.

 

7. Ninaenenda sasa kwa jina lake Yesu, salama nitafika nyumbani mwa Babangu. Lakini safarini naimba siku zote, nikimshukuru Mwokozi.

Nils Frykman, 1881




141 MWOKOZI wetu anatupa furaha duniani

 

1. Mwokozi wetu anatupa furaha duniani, atuongoza kwa neema na anatushibisha. 

Tazama, yupo pamoja nasi, neema haitaisha kamwe !
Haleluya, haleluya, haleluya amina!

 

2. Ni vema kumupenda mungu aliyetukomboa, vizuri kuwa mtu wake, sitapotea kwamwe.
Furaha yetu itabakia, ikiwa vyote vingetoweka.
Haleluya, haleluya, haleluya amina

 

3. Ikiwa giza mara nyingi, na jua likifishwa, na tukijaribiwa huku, twajua ni kwa muda.
Mbinguni hatutaona kamwe huzuni wala machozi tena.
Haleluya, haleluya, haleluya, amina

 

4. Na tusisumbukie tena chakula wala nyumba, maana vyote twavipata kwa ne’ma yake mungu!
Njiani yote atuongoza, aichukuwa mizigo yetu.
Haleluya, haleluya, haleluya, amina

 

5. Ikiwa vema huku chini kutegemea yesu, furaha gani huko juu kuona uso wake!
Tutaiona furaha tele, nutukufu hautaisha
Haleluya, haleluya, haleluya, amina!

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=VsU7u8L8tbg?feature=oembed&w=500&h=281]

______________________________________________________________________

 




146 KARIBU nawengu nilipotea njia

1. Karibu na wenzangu nilipotea njia, rohoni mwangu njaa, na sikuona raha, lakini sasa Yesu ni Mchungaji wangu, naandamana naye siku zote.

 

2. Katika shamba lake nimefuata Yesu, ninapajua anapolisha kundi lake. Na penye maji hai napunzika sana, naona raha hapo siku zote.

 

3. Lakini mchungaji apita vitu vyote, uzima aliweka kwa ‘jili ya kondoo. Nikumbukapo Yesu, sioni tena kitu cha kupendeza ila yeye, Bwana.

 

4. Naimba kwa furaha rohoni mwangu hivi: « Upendo wako, Yesu, ninausifu sana!» Na jina lake Yesu ni kama manukato; ananilinda vema siku zote.

Lewi Pethrus




157 HAIDURU kwangu uku chini

157

1. Haidhuru kwangu huku chini utajiri au umaskini, ila Bwana Yesu awe nami; ninatunzwa naye siku zote.

 

2. Haidhuru kama ninakuta shida nyingi katika safari, ila Mchungaji wangu mwema anilide na kuniongoza.

 

3. Haidhuru kama tunakaa katika baridi au hari, kwa sababu ukombozi wetu unakaribia. Haleluya!

 

4. Haidhuru kama sitapata utukufu na heshima huku; nikifanywa kama takataka, yanipasa kupendeza Bwana!

 

5. Haidhuru kama njia yangu inanichokesha mara nyingi, basi, nisigombane na ndugu, na pamoja tutashangilia!

 

6.Haidhuru kama tukiona sisi si wakubwa huku chini. Tuwe watumishi wake wema, na tutaingia kwake Bwana!

 

7.Haidhuru kama twasafiri katika dhoruba ya bahari, kwani Yesu ni nahodha wetu, atatufikisha bandarini.

Jonas Andersson




159 NASIKIA Bwana Yesu aniita ku’fuata

159

1. Nasikia Bwana Yesu aniita ku’fuata. Aliponitangulia nifuate yeye njia yote!

Pambio:
Nifuate nyayo zake, nifuate nyayo zake, nifuate nyayo zake, nifuate yeye njia yote!

 

2. Nifuate njia yote, na kwa maji nibatizwe, na kujazwa Roho wake! Nifuate Yesu njia yote!

 

3. Nifuate, nihubiri nelo lake la uzima kati’watu wa dunia! Nifuate Yesu njia yote!

 

4. Nifuate Bwana Yesu katika mateso, kufa, na nifufuliwe naye! Nifuate Yesu njia yote!

 

5. Atanipa ne’ma yake kwa kudumu hata mwisho, hata nitakapomwona Bwana Yesu huko ju’ mbinguni.

E.W. Blandley
I can hear my Saviour calling, R.S. 297




165 NITAZAMAPO kwa imani

165

1. Nitazamapo kwa imani Mwokozi wangu, nafurahi, naona utajiri wake anao Mungu, Baba yangu. Haleluya! Furaha kubwa, aniongoza siku zote! Nikiuona udhaifu, anichukuwa mikononi.

 

2. Sitasumbuka mimi tena, furaha inanijaliza; Na kwa upendo na rehema anisikia, nikiomba. Haleluya! Ananitunza, Ninastarehe kwa salama. Na ukitaka raha yake, mfungulie moyo wako!

 

3. Nilipokaa kati’ dhambi Nikaliona sikitiko, Lakini shaka na hukumu Zimeondoka kwangu sasa. Haleluya! Anipa nguvu Yakuyashinda majaribu. Rohoni mwangu nina raha, Nalindwa nayo siku zote.

 

4. Dhihaka na mateso yote si kitu kwangu kwa sababu nafarijiwa na Mwokozi, nakumbatiwa na babangu. Haleluya! Mwokozi wangu ananitunza kwa neema. Nikiwa na ‘dhaifu tena, natiwa nguvu kwa imani.

Samuel Gustavsson, 1930