107 ALIPOTESWA Yesu peke’ katika Gethemani




111 E’YESU sitasahau uchungu wako ‘kubwa

111

1. E’ Yesu, sitausahau uchungu wako kubwa, ulipoteswa Gethsemane usiku peke yako.

Pambio:
Mateso uliyoyaona, uchungu na machozi, Usiku ule Gethsemane, Siyasahau kamwe.

 

2.Naona wewe Gethsemane, ulivyoteswa huko kwa ‘jili ya makosa yangu, na kuitoa damu.

 

3.Huzuni nyingi uliona katika teso lako ulipoachwa peke yako na wanafunzi wako.

 

4.Na ukiona roho yangu haina pendo kwako, uniongoze Gethsemane, nione teso lako!

Edward P. Hammond
Tune: O Lord, remember me




113 MSALABANI Mwokozi wangu alijitoa kuniokoa

 113

1. Msalabani Mwokozi wangu alijitoa kuniokoa, na damu yake ilimwagika kwa’jili yangu, kunikomboa.

Pambio:
E’ Golgotha, e’ Golgotha, alipoteswa Bwana Yesu! E’ Golgotha, e’ Golgotha, nilipopata raha kweli!

 

2. Na nchi ile ilitetema, mbinguni jua likafunikwa wakati Yesu alipokufa, akichukua hatia yangu.

 

3. Likapasuka pazia lote, kwa hiyo neno limetimizwa. Naona njia ya mbingu wazi: Nikutakaswa kwa damu yake.

 

4. Mwokozi wangu, upendo gani: Uliutoa uzima wako! Kunikomboa ulisikia mateso yote ya msalaba.

William Darwood, 1886
On Calvary’s brow, R.S. 153




229 MWOKOZI Mfalme, ulisulubiwa

229

1. Mwokozu Mfalme, ulisulibiwa, e’pasaka wetu, ulidhihakiwa. Ukatoka damu, ‘kaona uchungu ulipotimiza mapenzi ya Mungu. Huku Gethsemane ulihuzunika, kwa neno la mbingu ukafarijika. Katika kuomba ukatiwa nguvu, na mwisho ukafa tupate wokovu.

 

2. Kwa ‘jili ya mimi ulijeruhiwa, ukaonja kufa, nipate uzima. Ulijisahau, ukanikumbuka, uliwaombea waliokutesa. Na ulijitoa dhabihu ya kweli, na kuusikia uchungu mkali. Kwa pendo kamili ulikusudia kuonja mauti kwa ‘jili ya wote.

3. Je, kupatanishwa na Mungu ni nini? Ni kwamba laana la dhambi lakoma. Kufika karibu na Mungu ni nini? Ni kuwa rafiki wa Mungu wa mbingu. Na sasa ufike kutoka dhambini, utie hatia na dhambi nuruni! Mwokozi mpendwa akuhurumia, atakufungua na ‘kusaidia.

Fr. E. Falk




231 MWOKOZI alitoa damu kwa’ jili ya waovu

231

1. Mwokozi alitoa damu kwa’jili ya waovu, msalabani alikufa kuniokoa mimi.

Pambio
E’ Yesu, niokoe sana, nifunze kuamini! Na unilinde tena, Bwana, nisipotee kamwe!

 

2. Alijitwika dhambi zetu, huzuni na maradhi; neema kubwa, wema wingi, upendo wa ajabu!

 

3. Na hapo jua likafichwa, ikawa giza kuu; muumba alitufilia kutulipia deni.

 

4. Magoti yangu nayapiga msalabani pake, na kwa machozi natazama mateso yake huko.

 

5. Nitakurudishia nini, Mwokozi wangu mwema? E’ Bwana, nikutumikie maisha yangu yote!

Isaac Watts
O Lord, remember me




291. MIMI mwenye hatiya nilikombolewa

 291

1. Mimi mwenye hatia nilikombolewa, Mwokozi alipojitoa. Dhambi zangu na zako alizichukua, kwa damu aliniokoa.

Pambio:
Dhambi zimetundikwa msalabani alipojitoa, Mwokozi. Alidharauliwa na kukataliwa atupatanishe na Mungu.

 

2. Yesu mwenye upole na mwenye upendo ananitakasa rohoni. Nimepata uhuru kwa Yesu Mwokozi, alikufa msalabani.

 

3.Namwambata Mwokozi, sitaki kumwacha, kwa kuwa alinifilia. Nakusifu, e’ Yesu, unayenipenda, daima nakushangilia.

Carrie E. Breck, 1855-1934
There was One who was willing to die in my stead, R.S. 737

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=qXvsR4Oo6io?feature=oembed&w=500&h=281]