287. TUNAMTIA mikononi mwako

287

1. Tunamtia mikononi mwako mtoto huyu, umtunze sana, na kila siku kwa neema yako umbariki, Bwana Yesu Kristo!

 

2. Ulimwengu kuna majaribu mahali pote, shida na mitego. Lakini uwe mchungaji wake, na umwongoze, E’ rafiki mwema!

 

3. Mwokozi kwa upendo ‘mchukue, asije akashindwa safarini! Na umlinde kwa rehema yako, apate kuwa wako siku zote!

 

4. Utume nuru ya neema kwake na maji ya uzima toka kwako e Bwana Yesu. Twakuomba leo ulinde mwana wetu kwa salama.

T.B. Barrat