9 NAIAMINI damu yako

1. Naiamini damu yako yesu na msalaba wako Yesu.
Mwokozi wangu wa pekee napata yote, Napata yote kwako.

Refrain : 
Uliyoyahidi Na’pata kwa imani.
Huwezi kuniacha mimi, Napata yote kwako
.

2. Kwa damu nimetasika, Namto wa uzima wako
waniletea nguvu tele, napate yote kwako.
 

3. Nafungwa kwa upendo wako, Njiani unaniongoza,
Na katika hatari zote napat nguvu kwako.
 

4. Ninakupenda, Bwana Yesu, Wanisikia niombapo,
Wanipa jibu la mombi Napata yote kwako.





11 IKIWA wananiuliza msingi wa uzima

1. IKIWA wananiuliza msingi wa uzima je?
twahitaji kuongeza kwa kazi yake Yesu?
Kwa uhodari nitajibu: msingi wangu ni wa nguvu,
ni damu yake Yesu Kristo inatosha sana.

 

2 UMWAMBA wa zamani sana, Daima utadumu.
Na hata siku nita’kufa, nitautegemeya.
Nitakapoondoka huku, nitaimbia majeraha
na damu ya mwokozi wangu, Funguo la mbingu.


 




24 E’MUNGU mwenye kweli

1. E’Mungu mwenye kweli, nakuamini sana, maneno yako yote, milele yata dumu ‘’niite kati’ shida nitakusaidia nategemea Bwana, ahadi yako hiyo.

 

2. Na katika uchungu ni heri kuamini kuamini, naweka roho yangu kulindwa nawe, baba, uliye nifundisha kuita jina lako; naona tumaini na tegemeo kwako!

 

3. Ninavyoomba kweli, najuwa wasikia. Yalioyo mema kwangu, najuwa wayafanya. Katuka shida kali waweza kunilinda; wanichukuwa mimi na masumbuko yangu.


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=RnHwRUNybAY?feature=oembed&w=500&h=281]




46 HAIFAI kuyasumbukia mambo yatakayokua kesho

46

1. Haifai kuyasumbukia mambo yatakayokuwa kesho. Baba yangu anajua yote, ni vizuri nikumbuke hivyo. Yeye mwenye moyo wa upendo ananipa yafaayo kweli, kama sikitiko au shangwe, na amani yake kila siku.

 

2. Siku zote yu karibu nami, na neema anapima sawa. Achukuwa masumbuko yote, yeye aitwaye Mungu Baba. Kunitunza hivyo kila siku, mambo hayo ame’tadariki. Kama siku, kadhalika nguvu! Ni ahadi niliyoipewa.

 

3. Mungu, unisaidie tena ‘kaa kimya kwako siku zote! Niamini sana neno lalo, ‘sipoteze bure nguvu yako! Nakatika mambo yote huku nipokee kwa mikono yako nguvu na neema yakutosha, hata nitakapofika kwako!

Lina Sandell-Berg, 1865




48 SIWEZI mimi kufahamu sana neema yake Mungu kwangu

 48

1. Siwezi mimi kufaamu sana neema yake Mungu kwangu, zamani nilikuwa mkosaji, lakini alinisamehe.

Pambio:
Bali namjua Mungu, anayeweza kunilindia urithi wangu juu hata siku yake Yesu.

2. Siwezi mimi kufaamu sana upendo wake ‘kubwa mno; nimeamini neno lake kubwa kweli, na ninaona raha tele.

3. Siwezi kufaamu kazi kubwa ya Roho yake ndani yetu, anayeweza kufundisha mtu kutegemea Yesu.

4. Sijui mimi siku zangu tena za kutembea duniani. Na labda nitaona shida huku, taabu na huzuni nyingi.

5. Sijui mimi kama siku moja nitakuona kufa huku, au kwa hima nitabadilika, ajapo Bwana na mawingu.

James Mc Granaham
I know not why, R.S. 617




50 SITASUMBUKA kwa kuwa Mungu ananitunza daima √√

50

Sitasumbuka kwa kuwa mungu ananitunza daima, anachukua mizigo yangu nyakati zote za mwendo.

Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo.

 

Sitasumbuka kwa kuwa mungu ni baba yangu kabisa, hawezi kunisahau mimi ingawa akijificha.

Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo

 

Sitasumbuka kwa kuwa mungu anishibisha neema, anipa yote yanifaayo kwa roho yangu na mwili.

Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo

 

Maua yote anayavika na ndege wote wa anga wanapokea chakula chao pasipo shamba na ghala.

Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo

 

Ninafurahi katika bwana, na kama ndege naimba. Najua kwamba nyakati zote babangu ananitunza,

Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo. 

________________________________________________________________________

 

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=MUrnWSHsEes?feature=oembed&w=500&h=281]



52 KWASALAMA baba awalinda watu wake

52

1. Kwa salama Baba Mungu awalinda watu wake, hata nyota za mbinguni si salama kama wao.

 

2. Mungu awalinda hivyo katika upendo wake. Wanakumbatiwa naye, wanarehemiwa sana.

 

3.Hawavutwi toka kwake kwa furaha wala shida. Yeye ni rafiki ‘kubwa wa walio watu wake.

 

4. Wanalishwa, wanavikwa, wanafarijiwa naye. Hata nywele za kichwani zimehesabiwa zote.

 

5. Enyi kundi lake dogo, Mungu atawahifadhi! Na adui watashindwa kwa uwezo wake ‘kubwa.

 

6. Akitoa, akiwapa, baba yetu hageuki. Na mapenzi yake ndiyo: Wana wapatishwe wema.

 

Lina Sandell-Berg, 1856


 

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=wDgmyqGOMz4?feature=oembed&w=500&h=281]



53 KATI’ mikono yake Yesu ananilinda katika pendo

 53

1. Kati’ mikono yake Yesu ananilinda. Katika pendo kubwa ninapumzika sana. Sasa sauti nzuri itokeayo juu inanikumbukia mbingu na raha yake.

Pambio:
Kati’ mikono yake Yesu ananilinda. Katika pendo kubwa ninapumzika sana.

 

2. Kati’ mikono yake nitakaa daima, sitatetema tena, yeye ni uwezo wangu. Shaka sinayo sasa, wala sioni woga, hata ikiwa shida, Yesu anifariji.

 

3. Yesu Mwokozi wangu alikombo mimi, Ufa wa mwamba ule, nitapumzika humo. Katika saa ngumu ya majaribu tele ninasaburi’ona jua la asubuhi.

Safe in the arms of Jesus, R.S. 663




54 USIOGOPE mateso yako

54

1. Usiogope mateso yako, Mungu anakulinda, bali tazama mapenzi yake,

Pambio:
Mungu anakulinda Mungu anakulinda siku kwa siku njiani mwake. Anakulinda salama. Mungu anakulinda.

 

2.Ukichukuwa mizigo ‘zito, Mungu anakulinda, kati’ hatari za njia yako Mungu anakulinda.

 

3. Anakumbuka hitaji zako, Mungu anakulinda. Utashiriki ujazi wake, Mungu anakulinda.

 

4. Katika njia ya migogoro, Mungu anakulinda. Mfunulie fadhaa zako, Mungu anakulinda.

Cevilla D. Martin, 1904
Be not dismayed, R.H. 458

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=Dl89FTY2gaU?feature=oembed&w=500&h=281]




78 NINAUZIMA wa milele

78

1. Nina uzima wa milele, na tumaini ni imara, mbinguni nitaona Yesu, Mwokozi wangu kwa furaha.

 

2.Nina urithi bora huko unaolindwa hata mwisho. Na kila siku ya jaribu natiwa nguvu naye Baba.

 

3.Namshukuru Mungu wangu! Ananitunza siku zote katika shida na taabu, kwa hiyo sisumbuki tena.

 

4. Rohoni mwangu ni amani, naimba kwa furaha kubwa. Nikiongozwa naye Yesu naendelea kwa salama.

 

5. E’ Bwana Yesu, unifunze ku’tumikia wewe vema wakati ubakio tena wa mwendo wangu dunianai!

Nils Frykman, 1883




96 MWOKOZI wetu aliahidi yakwamba atakuja siku moja kutupeleka

96

1. Mwokozi wetu aliahidi ya kwamba atakuja siku moja kutupeleka mbinguni kwake. Yawezekana upesi sana.

Pambio:
Sioni shida, nina amani kwa Mkombozi na damu yake, na Roho yake Mtakatifu ni arabuni ya ‘rithi yangu.

 

2. Wajumbe wengi wa Bwana Mungu watumwa sasa duniani pote. Waitangaza habari njema ya Yesu Kristo na pendo lake.

 

3.Na watu wengi wanaamini, wanaitika mwito wake Mungu. Kwa roho moja twa kaza mwendo, tufikilie thawabu yetu.

 

4. Twakaribia wakati ule wa kuja kwake Bwanda Yesu Kristo; na tujiweke tayari wote kuchukuliwa mbinguni kwake!

S.M. Linder, 1930




100 LO! Bendera inatwekwa

100

1. Lo! Bendera inatwekwa, yatutangulia! Tusione hofu, wenzi, twende kwa kushinda!

Pambio:
Bwana Yesu atakuja, tuilinde ngome! Kwa uwezo wake Yesu tutashinda yote.

 

2.Ibilisi azunguka, akitutafuta; anataka tuanguke, tufe, tupotee.

 

3. Vita kubwa, vita kali inaendelea, tuwe watu wa ‘hodari! Twende, tutashinda!

 

4. Basi, kwa bendera yake tunashikamana. Atutie nguvu yake hata kuja kwake!




115 PENDO la Mungu ni kubwa

115

1. Pendo la mungu ni kubwa, pasha habari hiyo! pendo la Mungu ni kubwa, mwanzo wa nyimbo zote. malaika waliimba wachunga wakasikia. tunafurahi kujua pendo la mungu ni kubwa.

refrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!

2. Pendo la mungu ni kubwa kwako uliye mbali. pendo la Mungu ni kubwa, anakuhurumia. ukiendee kisima kinachotoka golgotha, utaupata uzima katika pendo la mungu.

Refrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la mungu ni kubwa!

 

3. Pendo la mungu ni kubwa, latufikisha mbingu, pendo la Mungu ni kubwa, tutafurahi sana! huko hakuna jaribu wala ugonjwa na kufa. tumeokoka sababu pendo la mungu ni kubwa.

Pefrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!

4. Pendo la mungu ni kubwa, pasha habari hiyo! pendo la Mungu ni kubwa, mwanzo wa nyimbo zote. malaika waliimba wachunga wakasikia. tunafurahi kujua pendo la mungu ni kubwa.

Pefrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!

5. Pendo la mungu ni kubwa kwako uliye mbali. pendo la Mungu ni kubwa, anakuhurumia. ukiendee kisima kinachotoka golgotha, utaupata uzima katika pendo la mungu.

Pefrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!

 

6. Pendo la mungu ni kubwa, latufikisha mbingu, pendo la mungu ni kubwa, tutafurahi sana! huko hakuna jaribu wala ugonjwa na kufa. tumeokoka sababu pendo la mungu ni kubwa.

Pefrain:
Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=hYGGp7EtHUU?feature=oembed&w=500&h=375]

 




131 MIMI mukristu

131

1. Mimi mkristo nita’vyokuwa katika yote mpaka kufa. Mimi mkristo, ‘navyoshuhudu, dunia yote ikinicheka. Mimi mkristo kwa moyo wote sababu ninampenda Kristo, aliyekufa kwa ‘jili yangu. Anastahili kupendwa nami.

 

2. Mimi mkristo, neema kubwa! Niliokoka kutoka dhambi. Mimi mkristo, hata ikiwa katika shida na mapigano. Mimi mkristo, na ni askari, nafanya vita kushinda dhambi. Akida wangu ni Bwana Yesu, pamoja naye ‘tashinda yote.

 

3. Mimi mkristo, na ni mgeni, nimeifunga safari yangu; na sitamani yaliyo huku, ninatafuta yaliyo juu. Mimi mkristo na nchi yangu ni huku juu katika mbingu, hamna njaa na shida humo. Wakristo wote washiba mno

 

4. Mimi mkristo! Ni neno zuri la kufariji moyoni mwangu linanitwaa ju’ ya huzuni, nipumzike kwa Mungu wangu; Mkristo katika kila hali, na nikiitwa na kufa tena, kwa raha kubwa nitakubali kuchukuliwa mbinguni juu.

Joseph Grytzell, 1892




140 UKICHUKULIWA na mashaka yako

1. Ukichukuliwa na mashaka yako na kuona hufu kwamba utakwama, uhesabu mibaraka yake Mungu, na utashangaa kwa rehema yake.

Pambio:
Uhesabu mibaraka yote Mungu aliyoyakubariki! Ukumbuke mambo yote pia, na utashangaa kwa rehema yake!

 

2. Na ukiudhiwa na huzuni nyingi, ukiona msalaba ni mzito, uhesabu mibaraka kuchwa pia, na kwa moyo wote utasifu Mungu.

 

3. Wengi watamani mali ya dunia; utajiri wako ni Mwenyezi Mungu. Uhesabu mibaraka na kumbuka: Mali haiwezi kufungua mbingu.

 

4. Na katika mambo yote huku chini ukumbuke pendo kubwa la Mwokozi! Na ujumlishe mibaraka yote, tena mwisho atakuchukua kwake!

Johnson Oatman Jr
When upon life’s billows, R.S. 5


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=1VWWUGwVSTU?feature=oembed&w=500&h=281]

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=-zQDFxB8ZU0?feature=oembed&w=500&h=281]



147 MWENYEZI Mungu wazamani

1. Mwenyezi Mungu wa zamani zote ni kimbilio la vizazi vyote. Katika vita anawashindia na ku’okoa watu wake wote.

Pambio
Mfalme ‘kubwa ndiye Mungu, vitani anatushindia. Kwa shangwe kubwa tumsifu na tumwimbie Mungu wetu!

 

2. Mwenyezi Mungu wa zamani zote aliokoa watu utumwani, kwa njia kavu katika bahari wakafikishwa ng’ambo kwa salama.

 

3. Mwenyezi Mungu wa zamani zote Karmeli alishinda yule Ba’li, akasikia ombi la Eliya, ‘katuma moto juu ya sadaka.

 

4. Mwenyezi Mungu wa zamani zote akawa naye Daudi vitani; aki’tupia jiwe Goliati, shujaa alikufa mara moja

 

5. Mwenyezi Mungu wa zamani zote, uovu wote utashindwa naye. Atamseta yule mdanganyi, shetani, chini ya miguu yake.

 

6. Mwenyezi Mungu wa zamani zote atuongoza kwa mikono yake; anatulinda hatarini huku, mbinguni tutafika kwa salama.




150 NATAKA kupokea baraka yake Mungu

1. Nataka kupokea baraka yake Mungu, nataka kubatizwa kwa Roho ‘takatifu. Ju’ ya ahadi yake napumzika sana, aliahidi mimi kupata Roho yake.

Pambio:
Sawa na bahari, sawa na bahari ni neema yake anileteayo. Anayenijaliza, anayeniponyesha, ni Mwokozi wangu. Asifiwe sana!

 

2. Kanisa lake Mungu linaipata mvua, vijito vya baraka vinamiminwa sasa. Furaha ya uzima ni kubwa kati yetu. Tuimbe haleluya! Tumshukuru Yesu!

 

3. Mawimbi ya wokovu yanatujia sasa. E’ Mungu, tunaomba: Ujaze sisi sote! Watakatifu wako watakasike sana! Tuimbe haleluya! Tumshukuru Yesu!

 

4. Mawimbi ya wokovu yaliyofika kwetu, E’ Mungu, uyatume ulimwenguni mwote, maelfu kati watu wapate kuokoka, waimbe haleluya, wamshukuru Yesu!

H.J. Zelley, 1900
Like a mghty sea




154 E’RAFIKI shaka zako zipeleke kwake Yesu

154

1. E’rafiki, shaka zako zipeleke kwake yesu!
Aliyemwamini yey hataona haya kamwe.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

2. Dhambi zote ziungame na kwa damu utakaswe,
akuvike haki yake! Atakufikisha kwake.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

3. Masumbuko yako yote uyaweke mbele yake!
Ukipita uvulini, bwana yesu yupo nawe.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

4. Na furaha yako pia ijulike kwake yesu,
yeye bwana ju’ ya yote akubarikie yote!

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako

5. Ujitoe kwake yesu: roho, mwili na akili vyote vya
maisha yako anataka ku’takasa.

Refrain:
Naamini, naamini, ninakuamini, yesu. Naamini, naamini, naamini neno lako




155 KATIKA matumaini kwa Mungu wangu nakaa katika raha na utulivu

155

1. Katika matumaini kwa Mungu wangu nakaa katika raha na utulivu. Na yeye ni mwamba wangu, imara sana; katika dhoruba zote ananilinda.

 

2. Mwenyezi ni ngome yangu, sitatetema; siwezi kuhofu tena huzuni, shida. Ikiwa ni vita kali, sitaogopa; ni msaidizi wangu karibu nami.

 

3. Mahali pa kustarehe kwa Yesu Kristo; napata amani, raha, furaha kubwa. Faraja katika shida, gizani nuru, na katika pepo nyingi bandari nzuri.

Jonas Petersen
Allenast i hopp till Gud, Evgt. 1; M.A. 225




156 WALIAMINIO neno lake Mungu watapata nguvu kuwa washindaji

156

1. Waliaminio neno lake Mungu watapata nguvu kuwa washindaji, kwani Bwana Yesu alituahidi atathibitisha neno kwa ishara.

Pambio:
Shinda, shinda, nguvu ya kushinda! Shinda, shinda, shinda kila saa! Mungu atatupa nguvu ya kushinda, Tumtii Yesu nasi tutashinda!

 

2. Kati’ vita kali tuwe na ‘hodari, Mungu ndie nguvu yetu ya ajabu! Tu’amini neno: Na ishara kubwa ziatafuatana na waaminio.

 

3.Nguvu ya kupiga vita ya imani, nguvu ya kupinga hila za shetani! Yesu amesema: Na ishara kubwa zitafuatana na waaminio.

Leila Morris, 1862-1929
Theu who know the Saviour, R. H. 441




161 UMESHIRIKIANA naye Yesu? kama tawi ndani yake mzabibu?

161

1. Umeshirikiana naye Yesu kama tawi ndani yake mzabibu? Una raha iliyo timilifu, umejazwa Roho yake ‘takatifu?

Pambio:
Umeshirikiana naye Yesu kama tawi ndani yake mzabibu? Kuna raha na starehe katika kuomba Mungu; akutia nguvu ya kushinda yote.

 

2.Umepata imani ishindayo katika mashaka, shida huku chini? Umepata neema ya kudumu inayokulinda katika hatari?

 

3. Kwake Yesu mahali pa amani, huko ndiko pa kuburudika sana; atujaza mioyo utulivu, tunakaa na raha na starehe. 

 

4. Twafurahi kwa wema wake wote, twamsifu kwa ulinzi wake pia. Hata tukiudhiwa huku chini, atatufikisha kwake huko juu.

F.M. Lehman




164 IZRAELI wake Mungu

164

1. Israeli wake Mungu, kimya sana, wa’zunguka Yeriko kwa imani. Malaika wake aliwaongoza, na waliendelea kwa kushinda.

Pambio:
Twende kwa kushinda, twende kwa kushinda! Kwa damu yake Yesu, twende kwa kushinda! Tegemea Mungu, anatuongoza, na kwa imani, twende kwa kushinda!

 

2. Na Daudi, mchungaji, alikwenda mbele yake Goliathi bila woga; kwa imani alitupa jiwe lake, kwa jina lake Mungu akashinda.

 

3. Danieli aliomba kila siku, hakuhofu pango la simba kamwe; katika imani aliomba Mungu, akaokoka katika hatari.

 

4. Hata safarini huku kwenda mbingu nikipita katika jangwa kavu, na kupatwa na ‘jaribu mbalimbali, najua kwa imani nitashinda.

 

5. Na imani inashinda hali zote, inaruka juu ya mambo yote. Niliye dhaifu sitahofu kamwe, kwa kuwa Mungu ananiokoa.

William Grum




166 TUKIENDA pamoja

 166

1. Tukienda pamoja, tukishikamana na Mungu, tunapata amani na raha; tukifanya daima yanayompendeza, yu karibu kutusaidia.

Pambio:
Raha, furaha twazipata kwa Yesu, tukidumu katika kuamini, kutii.

 

2.Ikiwapo dhoruba, na mawimbi ya’vuma, yanakoma kwa neno la Yesu. Tukiona jaribu na kuhofu adui, tutashinda kwa nguvu ya Yesu.

 

3. Tukibeba mizigo anatustarehesha, tunapata furaha halisi. Masumbuko yatoka, giza inageuka kuwa nuru njiani mwa Mungu.

 

4. Tuna raha ya Mungu katika mashindano tukitii na tukiamini. Jua lake la pendo linawaangazia watiio na waaminio.

J.H. Sammis




168 NINA mshirika nafuraha kubwa

168

1. Nina ushirika na furaha kubwa, namtegemea Bwana Yesu. Wingi wa uheri kwa waaminio: Kustarehe mikononi mwake!

Pambio:
Raha, raha, raha kwa Yesu na amani! Raha, raha, nastarehe mikononi mwake.

 

2. Raha ya ajabu ni rohoni mwangu, namtegemea Bwana Yesu. Nuru huangaza njia niendayo; nastarehe mikononi mwake.

 

3. Woga na huzuni zinatoka kwangu, nikitegemea Bwana Yesu. Ninafarijiwa siku zote naye, nastarehe mikononi mwake.

E.A. Hoffman
What a fellowship, R.S. 377; R.H. 482; MA.




169 ASKARI wa imani sisi

169

1. Askari wa imani sisi, kwa shangwe tunaendelea, hata vita ‘kiwa kali tuna nguvu na ‘hodari. Tuna upanga wa imani, ni neno lake Mungu wetu; na kwa jina lake Yesu tunashangilia sasa.

Pambio:
Mbio tutaacha huku, vita ikiisha. Tutaingiamo mbingu ku starehe humo. Wao washindao huku, watapewa taji kwa mkono wa Mwokozi, anayewapenda.

 

2. Tuvae kila mtu sasa silaha zote zake Mungu. Na mishale ya shetani ‘tazimika mbele yetu. Tukimtii Bwana Yesu, twaendelea kwa ‘hodari, na kwa nguvu za ahadi tutakuwa washindaji.

 

3.Na ukipungukiwa nguvu, katika vita ukishindwa, Yesu atakutilia nguvu mpya ya kushinda. Kwa nyimbo za kushangilia, utahimili shida zote, na kupata kuokoa wenye dhambi na makosa.