96 MWOKOZI wetu aliahidi yakwamba atakuja siku moja kutupeleka

96

1. Mwokozi wetu aliahidi ya kwamba atakuja siku moja kutupeleka mbinguni kwake. Yawezekana upesi sana.

Pambio:
Sioni shida, nina amani kwa Mkombozi na damu yake, na Roho yake Mtakatifu ni arabuni ya ‘rithi yangu.

 

2. Wajumbe wengi wa Bwana Mungu watumwa sasa duniani pote. Waitangaza habari njema ya Yesu Kristo na pendo lake.

 

3.Na watu wengi wanaamini, wanaitika mwito wake Mungu. Kwa roho moja twa kaza mwendo, tufikilie thawabu yetu.

 

4. Twakaribia wakati ule wa kuja kwake Bwanda Yesu Kristo; na tujiweke tayari wote kuchukuliwa mbinguni kwake!

S.M. Linder, 1930