93 SIKU chache

93

1. Siku chache, na tena wakristo watakwenda kumwona Mwokozi, siku chache na wataipewa thawabu na taji ya uzima.

Pambio:
Nangoja sana Bwana Yesu kama zamu angojavyo asubuhi. :/: Kwa dalili zote ninaona sasa kwamba Yesu yu karibu ya kurudi:/:

 

2. Siku chache za vita ya huku, tena Yesu Mfalme atakuja; tutaona furaha na raha, atatupeleka kwake juu.

 

3. Siku chache machozi ya shida, Mungu atayafuta kabisa. Na baada ya siku si nyingi kwa lango nitaingia mbingu.

 

4. Baragumu la mwisho ‘talia, waminifu watachukuliwa; wote wataingia mbinguni kukaa pamoja na Mwokozi.

J.F. Thori

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=qByPCSUaE-o?feature=oembed&w=500&h=281]