78 NINAUZIMA wa milele

78

1. Nina uzima wa milele, na tumaini ni imara, mbinguni nitaona Yesu, Mwokozi wangu kwa furaha.

 

2.Nina urithi bora huko unaolindwa hata mwisho. Na kila siku ya jaribu natiwa nguvu naye Baba.

 

3.Namshukuru Mungu wangu! Ananitunza siku zote katika shida na taabu, kwa hiyo sisumbuki tena.

 

4. Rohoni mwangu ni amani, naimba kwa furaha kubwa. Nikiongozwa naye Yesu naendelea kwa salama.

 

5. E’ Bwana Yesu, unifunze ku’tumikia wewe vema wakati ubakio tena wa mwendo wangu dunianai!

Nils Frykman, 1883