Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

77 NAIFUATA njia ya ku’fikia mbingu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

77

1. Naifuata njia ya kufikia mbingu na mji mwema ule alio’jenga Mungu. Ninasafiri sasa kutoka duniani nifikie nchi hiyo ya raha na uzima.

Pambio:
Naifuata njia ya ku’fikia mbingu na mji mwema ule alio’jenga Mungu.

 

2. Sijauona bado uzuri wake bora wa mji wa mbinguni, usio na machozi; lakini siku moja, kwa shangwe ya milele nitamsifu Yesu katika mji ule.

 

3. Nifikapo mjini, mlango wake wazi, na hapo malaika watanikaribisha; shindano la dunia halitakuwa huko, na nitaona raha milele na milele.

No comments yet.

Leave a Comment