72 MIMI mgeni katika dunia

72

1. Mimi ngeni katika dunia, ninasafiri kufika mbinguni. Hata ikiwa hatari njiani, nitaishinda pamoja na Mungu. Kama Ibrahimu majaribuni nita’vyoshinda kwa nguvu ya Mungu. Nitavumilia nifike mbinguni, ndilo kusudi la moyo.

 

2.Nikitembea gizani kabisa mimi mnyonge pamoja na Yesu, na nikipita motoni, majini, nakusudia kufika mbinguni. Mungu ajua mapito jangwani, naye Mwenyezi atanifikisha. Nitavumilia nifike mbinguni, ndilo kusudi la moyo.

 

3. Tusisumbuke katika safari, tuwatazame wali’tangulia! Yesu Mwokozi alitukomboa, msalabani alitufilia! Naye atatufikisha mbinguni; hivi tuimbe kwa mda kitambo: tutavumilia tufike mbinguni, ndilo kusudi la moyo!