Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

71 NIMEKWISHA kuingia nchi nzuri ya ahadi

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

71

1.Nimekwisha kuingia nchi nzuri ya ahadi, nchi njema ya wokovu wake Mungu. Huko ni vijito vingi vya baraka na furaha, huko shida haifiki.

Pambio:
Nimekwisha kuingia nchi nzuri ya ahadi. Moyo wangu hufurahi, ninaishi kwa neema.

 

2.Nimefika kanaani, hapo ni urithi wangu, na sitaki kuondoka tena kamwe. Sasa nira ni laini na mzigo si mzito, Yesu ni furaha yangu.

 

3.Nimekwisha kuingia nchi ya amani kuu, hata mwili wangu unatiwa nguvu. Nchi hiyo ni ya raha na faraja imo pia, hapo tunaka’ salama.

 

4.Nime’ngia nchi hiyo, ndiye Bwana Yesu Kristo, ninakaa tatika urithi wangu. Kwa imani ninakunywa maji hai ya kisima, huku ni furaha kubwa.

 

5.Nitafika hata mbingu, nchi ya hazina yangu, dhambi na mateso hazitakuwako, wala giza ya usiku, wala sikitiko chungu, wala shida, wala kufa. Werner Skibsted

No comments yet.

Leave a Comment