Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

69 JE, Tutaonana tena huko ng’ambo ya Yordani

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

69

1. Je, tutaonana tena huko ng’ambo ya Yordani, na pamoja na wakristo ‘ona raha ya milele?

Pambio:
Tuonane, tuonane huko ng’ambo ya bahari! Tuonane kwa furaha, huko shida ikomapo!

 

2. Je, tutaonana tena, ba’da ya dhoruba zote huko katika bandari ya salama na amani?

 

3. Je, tutaonana tena kati’ mji wa dhahabu, Penye mto wa uzima nayo miti ya matunda?

 

4. Je, tutaonana tena na kusifu Mungu wetu miongoni mwa wakristo waimbao huko juu?

 

5. Tutaona na wapenzi waliotuacha huku? Je, tutawaona wote katika makao meme

 

6. Tutaona Bwana Yesu katika kutano huko, tutakaribishwa naye katika karamu kuu.

Th. Hastings

No comments yet.

Leave a Comment