67 TUNAKARIBIA kao la mbinguni

67

1. Tunakaribia kao la mbinguni, hata jua likifichwa na mawingu. Tufuate Bwana Yesu siku zote, ni furaha yetu kumwandama yeye!

Pambio:
Tunakaribia mbingu kati’ yote, haleluya! ‘sifuni Mungu! Jipe moyo safarini kwani Yesu yu pamoja nasi hata mwisho!

 

2. Tunakaribia kao la mbinguni, hata tukiona pepo na dhoruba. Bwana yu karibu, na uwezo wake ni makimbilio yetu hatarini.

 

3.Njia yetu inapita kati’ jangwa, na miguu inauma mara nyingi, walakini tunakwenda tukiimba na kusifu Yesu, Mwokozi wetu.

 

4. Mwendo wetu utaisha siku moja, tutapata kustarehe huko juu. Tukiona shaka, shida hapa chini, tutapata utulivu kwake Yesu.

Pambio:
Tunakaribia mbingu kati’ yote, haleluya! ‘sifuni Mungu! Tunataka kufuata hata mwisho. E’ rafiki, utuandamie!

Nathan Cronsie, 1914