Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

66 WAKRISTO wa nchi zote watakusanyika huko kwa Yesu

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

66

1. Wakristo wa nchi zote watakusanyika huko mbinguni kwa Yesu, mezani pake, kati’ ufalme wake; kuona uzuri wake, kujazwa neema yake. Wataimba huko ju’ milele na milele.

Pambio:
Watoka bahari zote, watoka katika shida, watoka milima, watoka mabonde kufika kwa Mungu Baba, kuvikwa mavazi safi, kuona Mwokozi wao, yeye ali’wafilia ju’ ya msalaba.

 

2. Watakusanyika wengi walikotoka huku. Mateso na kufa, shida na giza hawata’ona kamwe. Ya kale hayatakuwa, lo! yote ni mapya huko! Itakuwa raha tu pamoja na faraja.

 

3. Tazama mlango huko uliokufunguliwa, na kuna mahali Yesu aita: « Njoo nyumbani kwangu wenzetu waliofika wanatungojea huko, malaika wanaimba kukukaribisha. Amanda Sandbergh

No comments yet.

Leave a Comment