Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

65 HUKO ju’ ya nyota zote kuna chi yenye mema

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

65

1. Huko ju’ ya nyota zote kuna nchi yenye mema, Mji wake ni Yerusalemu; Dhambi haitakuwamo, wala kufa na huzuni, Kwake yesu nitapata kao.

Pambio:
Sikitiko na machozi hayatakuwako huko, Wala giza au vita ya dunia. Huko hatutayaona mambo ya kutuumiza. U Yerusalemu ‘takatifu!

 

2.Nifikapo mji huo nitaona Yesu kwanza, aliyechukua dhambi zangu. Nitaona uso wake, nitamshukuru yeye aliyeniweka huru kweli.

 

3.Huko nitaona tena jeshi la walioshinda kwa imani huku duniani, na pamoja nao wote nita’sifu Mungu sana juu ya neema yake kubwa.

No comments yet.

Leave a Comment