63 YESU nivute karibu nawe
63
1. Yesu, nivute karibu nawe, ‘kiwa kwa shida, ikiwa kwa raha! Uliyekufa msalabani, :/: ‘nifaamishe upendo na ne’ma! :/:
2. Yesu, nivute, mimi maskini, sina vipaji vya kukutolea, moyo ninao wenye udhaifu, :/: Uupokee, ‘uoshe kwa damu! :/:
3. Yesu, nivute, nikutolee yote ninayo, e’ Bwana mpendwa, ninakuomba: Uyaondoe :/: yote yanayo nitenga na Mungu! :/:
4. Yesu, nivute karibu nawe hata ukomo wa vita na shida! Tena mbinguni nitakuwapo :/: karibu nawe, e’ Yesu Mwokozi! :/:
Leila Morris, 1862-1929