61 ENYI wetu wa Sayuni

61

1. Enyi watu wa Sayuni, kundi dogo la Mwokozi, Yesu aliwanunua kuwa mali yake Mungu. Sasa mnapita njia ya miiba na hatari kati’ nchi ya ugeni; bali mbingu mtafika.

 

2. Kumwamini, kumpenda Yesu ni uheri wetu; amri zote zinashikwa kwa upendo na amani. Kwa imani twaokoka, pendo ni uzima wetu. Yesu utusaidie, utujaze pendo lako!

 

3.Juu ya msingi huo, Yesu, unijenge mimi, na zaidi niungane nawe na kanisa lako! Sisi tu matawi yako, tushirikiane sana, na katika kundi nzima iwe nia moja kweli!

A.C. Rutström