57 YESU uliye kufa kwa ajili yangu

 57

1. Yesu, uliyekufa kwa ajili yangu, ninajitoa kwako, niwe mali yako! Bwana, nivute kwako, nifaamishe pendo, niwe dhabihu hai katika shukrani!

 

2. Yesu, nafika kwako, kao la rehema; Bwana, nitie nguvu kwa neema yako! Niuchukue tena kwa radhi msalaba, ni’tumikie wewe, Mkombozi wangu!

 

3. Bwana, uniumbie moyo haki, safi, kwako niishi tena hata kufa kwangu! Niwatafute wenye dhambi na udhaifu, niwapeleke kwako, Bwana wa upendo!

 

4. Vyote ninavyo huku nimepewa nawe, ukivitaka, Bwana, uvitwae vyote! Nina urithi wangu kwako mbinguni juu, nitakuona huko kwa furaha kuu!

S.D. Phelps, 1862
Evgt. 81More love to Thee,, o, Christ, R.S. 959