51 NAONA amani Golghota alipo jitoa Mwokozi

51

1. Naona amani Golgotha alipojitoa Mwokozi,
:/:Na huko nina kimbilio kwa Yesu aliyejitoa.:/:

 

2. Sitaki ‘tamani fahari na dhambi katika dunia,
:/: Sababu wokovu ninao katika ‘jeraha ya Yesu. :/:

 

3. Aliziondoa kabisa mizigo na kamba ya dhambi.
:/: Na niliokoka halisi kwa neno la Mungu wa ‘hai. :/:

 

4. Maneno ya Mungu ni kwetu chakula na dawa ya roho,
:/: na nguvu ya kusaidia mkristo katika safari. :/:

 

5. Mimi sasa hekalu la Roho, anayemiliki moyoni;
:/: na Yesu ataniongoza kwa njia ya ahadi zake. :/:

 

6.Uliye dhambini ufike kwa Yesu Mwokozi wa wote!
:/: Anakunyoshea mikono ya pendo kukusaidia. :/: