50 SITASUMBUKA kwa kuwa Mungu ananitunza daima √√
50
Sitasumbuka kwa kuwa mungu ananitunza daima, anachukua mizigo yangu nyakati zote za mwendo.
Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo.
Sitasumbuka kwa kuwa mungu ni baba yangu kabisa, hawezi kunisahau mimi ingawa akijificha.
Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo
Sitasumbuka kwa kuwa mungu anishibisha neema, anipa yote yanifaayo kwa roho yangu na mwili.
Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo
Maua yote anayavika na ndege wote wa anga wanapokea chakula chao pasipo shamba na ghala.
Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo
Ninafurahi katika bwana, na kama ndege naimba. Najua kwamba nyakati zote babangu ananitunza,
Refrain:
Sijaiona nyingine siku jana imetoweka na leo mungu anazijua hitaji zote ninazo.
________________________________________________________________________