45 WAIZRAELI walika’ Babeli utumwani

45

1. Waisraeli walika’ Babeli utumwani, wakawa na huzuni tu kwa ‘jili ya sayuni.

Pambio
Hapo amri ilifika waliweza kuondoka, shangwe gani mioyoni mwao! Walitwaa vinubi vyao, wakaenda wanaimba hadi, hata kurithi nchi yao.

 

2. Vinubi havikubigwa wakati wa utumwa, na walikaa kimya tu mahali pa ugeni.

 

3. Walipotoka Babeli, ikawa kama ndoto; furaha nyingi rohoni, faraja na uheri.

 

4. Mataifa walisema: «Mungu umefanyaje? Watumwa wameondoka, wamewekwa huru»!

 

5. Katika ulimwengu hu’ ni wengi wafungwao. Uhuru ni kwa Yesu tu kwa kila a’miniye.

Pambio:
Ndiye ameleta amri: Tunaweza kuokoka, shangwe ku’kwa kila ‘aminiye! Njoo sasa, twa’ kinubi, tufuate kwa kuimba hata kuirithi nchi yetu!

Werner Skibstedt