Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

44 Tu watu huru

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

44

1. Tu watu huru, huru kweli katika Yesu Kristo. Tunahubiri neno lake kwa moto ‘takatifu. Tuendelee, mbele, mbele, tukashinde majaribu! Twapiga vita ya imani, tuvumilie yote!

 

2. Tu jeshi kubwa la askari, tu safi kati’ damu. Mfalme wetu, Yesu Kristo, ni kiongozi wetu. Kwa nguvu yake kubwa mno tutadumu hata kufa.Tuendelee, mbele, mbele, tumshukuru Mungu.

 

3. Kwa Yesu tuna uhodari na mamlaka kubwa, maana tunayaamini maneno yake yote. Kisima wazi, cha ajabu, kinatoka msalaba, tuliyakunywa maji yake, ni maji ya uzima.

 

4. Mbinguni nchi ya asili [raha], ya haki na amani, tuta’pofika huko juu tutamwimbia Yesu. Na kila chozi litafutwa na mkono wa Mwokozi. Kwa shangwe kubwa tutarithi ufalme wa ahadi.

Werner Skibsted

No comments yet.

Leave a Comment