40 AMENIWEKA huru kweli

40

1. Ameniwaka huru kweli, naimba sasa: Haleluya! Kwa msalaba nimepata kutoka katika utumwa.

Pambio:
Nimeokoka, nafurahi! Na dhambi zangu zimetoka. Nataka kumtumikia Mwokozi wangu siku zote.

 

2. Zamani nilifungwa sana kwa minyororo ya shetani, nikamwendea Bwana Yesu, akaniweka huru kweli.

 

3. Neema kubwa nilipata kuacha njia ya mauti, na nguvu ya wokovu huo yanichukua siku zote.

 

4. Na siku moja nitafika mbinguni kwake Mungu wangu. Milele nitamhimidi na kumwimbia kwa shukrani.

 

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=1s24X-6Hv2k?feature=oembed&w=500&h=375]