37 BWANA Yesu aliniokoa kweli

37

1. Bwana Yesu aliniokoa kweli, ninataka kufuata yeye sasa. Kila siku nimtumikie vema, yeye anipaye roho kwa neema!

Pambio:
Nafuata njia nzuri ya Mfalme Yesu Kristo, Na katika njia hiyo Mwendo ni pamoja naye.

 

2. Sitaifuata njia mbaya tena, nimewekwa huru kweli naye Yesu. Kumtumikia ni furaha yangu, ananishibisha kwa fadhili zake.

 

3. Huko mbele ninaona mji mwema, nimeacha njia ndefu nyuma yangu. Nuru ya Babangu yaniangazia, nitembee kwa salama siku zote.

 

Henri Dixon Loes