35 NIMEFIKA kwake Yesu

35

1. Nimefika kwake Yesu, Na rohoni mwangu sasa, jua lake la neema linang’aa kila siku.

Pambio:
Roho yangu inaimba, nimefunguliwa kweli. Nimekaribia Yesu, ninaimba kwa furaha.

2. Pepo za neema yake zinavuma ndani yangu, na mawimbi ya wokovu yananijaliza sasa.

3. Sasa Bwana Yesu Kristo amefanya kao kwangu. Nimepewa mfariji, Roho ya ahadi yake.

4. «Siku roho afikapo mtajua kwa hakika kwamba ninakaa kwenu», hivyo Yesu alisema.

5. Kweli, amefika kwetu, sasa yumo ndani yetu. Ujitoe kwake Mungu, aioshe roho yako!

6. Yesu atakapokuja katita utakatifu, nitafananishwa naye, nitamshukuru sana.

Pambio:
Zitakuwa nyimbo nyingi tuta’poingia mbingu, na milele tutaimba na kusifu Mungu wetu.

Werner Skibsted