Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

34 KWA pendo lake kubwa alitafuta mimi

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

34

1. Kwa pendo lake kubwa alitafuta mimi, na alinichukua begani mazizini na nyimbo zao malaika zikajaza mbingu pia.

Pambio:
Alinitafuta, akaniokoa, akaniondoa matopeni, akanichukua mazizini.

2. Mchunga mwema Yesu aliniponya roho, na akaniambia: «Mtoto upendwaye». Sauti yake ya upendo ikaufariji moyo.
3. Ninakumbuka jinsi alivyotoka damu, na taji ya miiba, mateso ya mauti. Na penye msalaba wake ninashukuru Bwana Yesu.
4. Namfuata yeye katika nuru yake, waridi za ahadi zapamba njia yangu. Milele nitaendelea kusifu Yesu kwa furaha
5. Na saa zinapita, nangoja asubuhi utakaponiita, niende kwako juu. Nitasimama kwa amani mbinguni mbele yako, Yesu.

W. Sencer Walton

No comments yet.

Leave a Comment