33 HURU kama ndege bustanini

33

1. Huru kama ndege bustanini, sasa nafurahi kwa sababu Yesu ni rafiki yangu ‘kubwa; nina amani siku zote.


2. Aliniokoa na mashaka, alinipa tunu ya rehema. Mimi ni mtoto wa babangu, na nuru inang’aa sana.


3. Ninataka ku’shukuru Bwana, alitupa dhambi zangu mbali, na sitaziona tena kamwe, hazitanitawala tena.


4. Jua likifichwa kwa mawingu, kiti cha rehema ni karibu, hayo ndipo shida ziishapo, na roho yangu yatulia.


5. Radhi kama mwana kwa babake, kwa salama kama bandarini, Ninapumzika kwa Mwokozi, mbali na shida na huzuni.


6. Yesu yu karibu siku zote, achukua mimi na mzigo. Napokea kwa mkono wake neema na mateso pia.


7. Nilimpa Yesu moyo wangu, ninapenda kumtumikia; neno lake linapendwa nami, na nira yake ni laini.


8.Nafurahi sana kanisani kati ya watoto wa babangu, Roho ya neema ni karibu, kunanifurahisha sana.


9. Mimi ni mdogo duniani, tena msafiri na mgeni. Kwetu ni mbinguni huko juu; babangu ananiongoza.


10. Saa za mashaka zitakwisha, kuja kwake Yesu ni karibu. Nitaona raha kubwa sana katika nyumba ya babangu.

Nils Frykman