329 Ewe Mwana wa Mungu, niokoe nami

1. Ewe Mwana wa Mungu, niokoe nami, nikutumikie na niende Sayuni. (2x)

Pambio:
:/: Sifa zina wewe, Sifa zina wewe, Sifa zina wewe, Milele na milele.:/:

 

2. Mavuno ni mengi, watenda kazi ‘chache. Ita wengi Bwana, waingie kazini. (2x)

 

3. Tuombe kwa bidii Bwana wa mavuno, atume watumishi kati shamba lake. (2x)

 

4. Bwana Yesu yu aja, na ujira wake, kulipa watumishi kama kazi zao. (2x)

WATONGOKA Mulonge Erasto, 1964

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=IZbVs56tJFo?feature=oembed&w=500&h=281]