327 Katika giza la usiku, pakawa na kelele kuu

1. Katika giza la usiku, pakawa na kelele kuu. Tazama Bwana yu karibu, tokeni mwende kumlaki.

:/: Tazama, Bwana yu karibu, Tokeni mwende kumlaki. :/:

2. Na wanawali wote kumi, wakachukua taa zao. Lakini tano wapumbavu wapungukiwa na mafuta. 3. Wakawasihi wa busara, tupeni kwa mafuta yenu. Zinazimika taa zetu, na hatujui tutendalo.

4. Wakawajibu wa busara, hayatutoshi sisi nanyi. Mwendeni kwao wauzao mkajinunulie sasa.

5. Na wakaenda kununua, akaja Bwana wa arusi. Watano walio tayari wakaingia arusini. 

6. Mlango hapo ukafungwa, halafu wale wapumbavu wakaja nao, wakalia, tufungulie, Bwana wetu.

7. Bwana arusi akajibu: amina, siwajui ninyi. Kesheni basi, kwa sababu hamjui siku yangu.

:/: Tazama, Bwana yu karibu. Jitayarishe kumlaki.:/:

8.Gizani, nje ya arusi, wakasimama wapumbavu. Kulia wakalia sana, tufungulie, Bwana wetu.

:/: Na jibu likatoka wazi: Mmechelewa kuingia. :/: