Digg StumbleUpon LinkedIn YouTube Flickr Facebook Twitter RSS Reset

32 HAPO nilikua chini katika dhambi nyingi

image_pdfsauvegarder en PDF-Saveimage_printImprimer-Print

32

1. Hapo nilikuwa chini Katika dhambi nyingi, roho yangu iliona kufa na giza tele. Mungu alikisikia kilio changu huko, naye akanipandisha, kuniponya.

Pambio:
:/: Nimeokoka, nimeokoka! Yesu Mwokozi wangu aliniokoa:/:

2. Sasa Yesu amekuwa makimbilio yangu, na upendo wake ‘kubwa uko moyoni mwangu. Ne’ma yake kubwa sana inajaliza roho, niwe mwaminifu kwake siku zote!

3. Ewe, mwenye sikitiko, kuna matumaini: Yesu anakufahamu, atakusaidia. Atakupandisha toka tope la kuteleza, upokee ne’ma yake kwa wokovu!

James Rowe, 1912

No comments yet.

Leave a Comment