318 Nimeliona pendo kubwa mno

1. Nimeliona pendo kubwa mno, na pendo hilo nalifurahia. Na jina lake mwenye kunipenda, Ni Mungu Baba tena Yesu Mwana. :/: Upendo wako nausifu sana, ewe Mungu nawe Yesu Kristo. :/:

 

2. Mimi mtoto mdogo mbele yako, nakuhitaji unisaidie. Kwa kila kazi na kwa hali zote, kwa majaribu katika dunia. :/: Usiniache mimi peke yangu, uwe nami kwa safari yangu. :/:

 

3.Nikikuomba uje kwangu Yesu, ukija tena ninaona hofu. Utanishika mimi mwanadamu, sitendi vema mimi mwenye shaka. :/: Nilipendalo silitendi tena, ninafanya nisilolipenda. :/:

 

4.Nilipokuwa mtoto mchanga, na niliwaza mambo ya utoto. Na kwa wakati wakuwa mzima, nilibadili mambo ya utoto. :/: Matumaini na imani yangu, inakwamilishwa kwa injili. :/:

 

5.Nimeliona pendo la Mwokozi, aliyenikomboa kati damu. Na damu hiyo si damu ya nyama, ni damu yake Bwana Yesu Kristo. :/: Ee! Mwenye haki kwa wasio haki, umetoa maisha na pendo.:/:

TAMBI Eae Munaongo, 1942