317 Sisi tuliokoka na tunashangilia

1. Sisi tuliokoka na tunashangilia, twapita unlimwengu na tuna amani.

 

2. Mwapenda vya dunia mbona hamvishibe, hata wababu zenu hawakuviweza.

 

3.Dunia itaisha na vyote vilivyomo. Nyumba na mashamba, akili na pombe.

 

4. Vinavyowadanganya havitawaokoa, vitakuwa majivu, arudipo Bwana.

 

5. Na wenye roho ngumu, tuwafanyie nini? Mbona tunawaonya na mnakataa?

 

6. Hatuna la kufanya, tutahamia mbingu. Tunasikitika ju’ ya wenye dhambi.

 

7. Tutakwenda mbinguni, kuona wateule, vijana ‘takatifu waliotakaswa.

 

8. Tutashirikiana na makabila tena, ila waliotubu na kuoshwa na Yesu.

 

Wimbo wa kirundi
TAMBI Eae Munaongo, 1952