315 Baba Mungu akifunga, hata moja tafungua

1. Baba Mungu akifunga, hata moja tafungua. Na kama akifungua, wakufunga anakosa. Siku utatufungua tutaruka kama njiwa, Eh Mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyake Mungu.

 

2. Sisi watumishi wako, umetuachia kazi. Ili tuifanye kwa bidii na tungoje kuja kwako, watumishi wako Bwana. Tunaomba utulinde, Eh Mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyake Mungu.

 

3. Mara nyingi tunaona uchokozi wa dunia, kutupima roho zetu, kwa kutesa mwili wetu. Haleluya tutasifu Mkombozi wetu Yesu, eh Mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyake Mungu.

TAMBI Eae Munaongo, 1952