313 Kumbe wakati wapita mbio, ni sawa jana mlipofika,

1. Kumbe wakati wapita mbio, ni sawa jana mlipofika, mlitumika pamoja nasi, na sisi wote tulifurahi.

 

2. Na kazi yenu tuliipenda, hamkuchoka kutufurahisha. Taabu yenu haiko bure, ni Bwana Yesu atawalipa.

 

3. Mnaporudi mlikotoka twaomba Mungu mrudi tena. Kutumika pamoja nasi, kazi ni nyingi zinazowangoja.

 

4. Machozi mengi yalengalenga kwa macho yetu mnapotuacha, ni siku gani tutaonana. Mwenyezi Mungu ndiye ajua.

 

5. Salamu sana kwa nchi yenu, kwa makanisa na wakristo, sema Mwokozi ni Yesu peke, aliyekwisha kutusamehe.

 

6. Pasha habari ya ile hati ya mashitaki imetundikwa na imekazwa kwa nguvu sana, msalabani ifedheheke.

 

7.Na ile hati ya adui, ni Bwana Yesu ameifuta, hakuna tena hukumu kwetu tunaokaa ndani ya Yesu.

TAMBI Munaongo, 1955