312 Zaburi 117:1-2

1. Zaburi 117:1-2. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, enyi watu wote mhimidi. Maana fadhili zake, kwetu sisi ni kuu, na uaminifu wa Bwana ni wa milele.

Pambio:
Zaburi 118: 1-7,2. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema. Kwa kuwa fadhili zake ni za milele. Israeli na aseme sasa, ya kwamba fadhili zake, ya kwamba fadhili zake ni za milele.

 

2. Mlango wa Haruni na waseme sasa, ya kwamba fadhili zake ni za milele. Wamchao Bwana na waseme sasa, ya kwamba fadhili zake ni za milele.

 

3. Katika shida yangu nalimwita Bwana. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; mwanadamu atanitenda nini? Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, msaidizi wangu.

TAMBI Eae Munaongo, 1958