311 Mara kwa mara Yesu aita, umwitikie sasa.

1. Mara kwa mara Yesu aita, umwitikie sasa. Yawezekana ni mara mwisho, anakuita sasa.

Pambio:
Wewe uliye dhambini, Yesu akutafuta. Akusamehe makosa, usichelewe ndugu.

 

2. Machangamko ya kidunia hayatakupata (sic) raha. Na mapendezo ya wenye dhambi yakudanganya sasa.

 

3.Giza ya kufa huja upesi, siku usipojua. Rafiki yangu usichelewe, kumpokea Yesu.

 

4. Roho ikiwa nzito na dhambi, Yesu anakujua. Akupokea vile ulivyo, tena utaokoka.

 

5. Mwito wa Mungu unakujia, mara kwa mara ndugu. Ukikataa kumpokea, utapotea kweli.

Missionnary, 1954