307 Walikombolewa waimba juu

1. Walikombolewa waimba juu, wakisujudu mbele zake Bwana. Huzuni na taabu zake dunia Bwana amewaondolea zote.

Pambio:
Wanamwimbia Mwana Kondoo aliyekufa, sasa yu hai, ameyashinda mauti.

 

2. Wanashika vinubi mikononi wakiimba wimbo wa Mwana Kondoo na Musa mtumishi wake Mungu, wakifurahia kushinda kwake.

 

3. Wasiopenda kumsujudia, katika dunia hii ya sasa. Hawataonekana mbele zake, watateketea motoni kweli.

 

4. Mda unaobaki ni mfupi, tujitayarisheni ndugu sasa. Bwana ajapo tuwepo tayari, tutaimba naye kule mbinguni.