306 Ninakuhitaji Mwokozi, kujazwa na Roho yako

1. Ninakuhitaji Mwokozi, kujazwa na Roho yako. Mapema, mchana, jioni, nikutumikie Yesu.

Pambio:
:/: Ninakuhitaji Yesu, nijazwe upendo wako. Na siku kwa siku, Mwokozi, nikutumikie vema. :/:

 

2. Ikiwa ni siku za kazi, ikiwa ni siku kuu. Ninakuhitaji Mwenyezi, kujazwa na Roho yako.

 

3. Nyumbani mwa baba na mama, kondeni mwa watu wengi. Popote ninapopitia, nilinde na niongoze.

 

4. Ninakuhitaji, Mwokozi, katika maombi yangu. Niombe kwa mapenzi yako, nipate yanifaayo.

 

5. Katika kitabu cha Mungu, twasoma ahadi zake. Aombaye atapewa, kwa jina la Yesu Kristo.

Missionnary