301 Njioni (sic) tumwimbie Bwana

1. Njioni (sic) tumwimbie Bwana tumfanyie shangwe kuu. Mwamba wa wokovu wetu, tuje kwake na shukrani, tumfanyie shangwe kuu, Bwana ni Mungu mkuu, na Mfalme wa wafalme, tena Bwana wa mabwana.

 

2. Mikononi mwake zimo bonde zote za dunia. Na vilele vya milima ndiye aliyezifanya, aliifanya bahari na nchi akaiumba, njioni (sic) wote tuabudu, tusujudu Mungu wetu.

 

3. Tupige magoti yetu mbele ya Muumba wetu. Kwani ndiye Mungu wetu nasi tupo mali yake, na kondoo zake yeye, ingekuwa heri leo, msikie neno lake msifanye mioyo gumu.

 

4. Kama huko kwa Moria siku za Munga jangwani. Hapo walinijaribu babu zenu hapo kale. Wakanipima kuona matendo yangu makuu, kwa miaka arobaini nikahuzunishwa nao.

 

5. Nikasema watu hawa waliopotoka mioyo. Hawakuzijua njia zangu niliwaonyesha, nakaapa kwa hasira yangu na kusema hivi: Wasiingie rahani mwangu ya huko Kanaani.

Yakobo Sulemani, 1971