299 JE, umelisikia jina zuri

299

1. Je, umelisikia jina zuri, Jina la Mwokozi wetu? Linaimbiwa duniani pote na katika watu wote.

Pambio:
Yesu, jina hilo linapita majina yote kwa uzuri! Ni lenye nguvu ya kutuokoa na hatia na makosa.

 

2. Linafariji moyo wa huzuni, latutia raha kuu. Katika shida na hatari huku jina hili latulinda.

 

3. Katika giza huku jina hili linang’aa kama nyota, lanipa utulivu na ‘hodari siku zote hata kufa.

 

4. Majina yote yasahauliwa, ila jina lake Yesu milele litang’aa huko juu. Yesu, jina nzuri mno!

Allan Törnberg, 1935