296. Dhambi hatia zimeondolewa

296

1. Dhambi, hatia zimeondolewa, yote ya kale yamepita sasa. Damu ya Yesu imenisafisha; ninamfurahia Mkombozi wangu.

Pambio
Mavazi safi na kao nzuri ninayo huko ju’ mbinguni. Thawabu nita’pewa huko ni taji ya uzima. Na Yesu ni Mwokozi wangu. Alinikomboa, alilipa deni langu. Pendo lake kubwa nina’sifu siku zote, ninamfurahia Mkombozi.

 

2. Siku za manung’uniko zimekwisha, nimeokoka katika utumwa. Sasa naona raha na furaha sababu Bwana Yesu alinikomboa.

 

3. Shaka na hofu zimeondolewa, na siogopi kufa kwangu tena. Katika Yesu ninatumaini. Na ninalindwa vema naye siku zote.

 

4. Roho wa Mungu amenijaliza, anifariji katika mwenendo. Yesu Mwokozi yu karibu nami, aliye ngao yangu na makimbilio.