295. E’FURAHENI watu wake Mungu

295

1. E’, furahini watu wake Mungu! Mwokozi wetu alituokoa. Neema kubwa, pendo la ajabu! Tusifu Mungu sana siku zote!

Pambio:
E’ Mungu ana mamlaka yote, ni ngao na makimbilio yangu; Ni Baba yangu, na anasikia maombi yangu. Asifiwe!

 

2. E’, furahini watu wake Mungu! Tuimbe nyimbo za furaha nyingi! Tusiogope ila tumwamini na twende mbele kwa uweza wake!

 

3. E’, furahini watu wake Mungu! Tukimahangilia (sic) Mungu wetu, jirani zetu wasioamini watatamani kumjua Yesu.

 

4. E’, furahini watu wake Mungu! Mfalme wetu yu pamoja nasi. Kitambo bado- na tutahamia mbinguni kwake Mkombozi wetu.