29 UNIVUTE Yesu

29
1. Univute, Yesu, nifuate nyayo zako, ‘kiwa kwa rafiki au katika wageni, na mahali pa furaha au sikitiko; sina budi kumkaribia Yesu.

Pambio:
Nimfuate, nimkaribie, siku zote na popote nimwandame Yesu! Nimfuate, nimkaribie, Yesu mbele, nami nyuma, hata mwisho!

2. Juu ya milima nitasikiliza Yesu, hata mabondeni nitaandamana naye. Jua, giza, afya, ‘gonjwa, utulivu, vita, kati’ hayo yote Yesu yu karibu.

3. Nikiteka maji, au nikilima shamba, nikika’ nyumbani au ‘kiwa safarini, hata huko soko neno moja ni halisi: Sina budi kumkaribia Yesu

Down in the valley, R.H. 245