286. YESU ulikaribishwa arusini

286

1. Yesu, ulikaribishwa arusini huko Kana; hapo ikadhihirishwa nguvu yako kwa ishara.

 

2. Leo tunakuhitaji, wabariki ndugu hawa: Bwana na bibi-arusi! Ndoa yao iwe sawa!

 

3. Katika taabu, raha, wafungane kwa upendo! Watumike kwa furaha, w’andamane kati’ mwendo!

 

4. Yesu, U mlinzi wao, uwalinde na mabaya! Uhifadhi nyumba yao! Tunaomba mema haya!

C.G. Lundin