284
1. Usimtafute Yesu kati’ wafu kaburini! Yu mzima, tumsifu, hakushindwa na kuzimu!
:/: Yesu hai, Yesu hai, mshindaji wa mauti! :/:
2. Maadui walifunga Bwana Yesu kaburini, Mungu alimfufua Mwana wake. Furahini!
:/: Yesu hai, Yesu hai, imba hivyo duniani! :/:
3. Yesu hai, ni habari ya kupasha pande zote. Yu Mwokozi wetu kweli, alitufilia sote.
:/: Yesu hai, Yesu hai, Mkombozi asifiwe!:/:
P.P. Bliss