283. NIMEYASIKIA mengi aliyoyafanya Yesu

283
1. Nimeyasikia mengi aliyoyafanya Yesu katika maisha yake huku chini: Pote alitenda mema, alisaidia wote. Kwa furaha ninaimba: “Yesu yeye yule leo!”

Pambio
Yesu Kristo yeye yule jana, leo, siku zote. Hutafuta wapotevu, huokoa na waovu. Mwokozi wetu yeye yule!

 

2. Na kipofu yule, jina lake ndilo Bartimayo, aliposikia Yesu yu karibu, kwa imani akaomba, akapona kwa neema. Nafurahi kwa kuimba: “Yesu yeye yule leo!”

 

3. Watu wote wenye dhambi na wagonjwa na maskini wanaitwa kwake Yesu kwa rehema. Uiguse nguo yake, sawa mwanamke yule, utapewa nguvu yake, kwani Yesu yeye yule!

 

4. Nimeyasikia tena jinsi alivyoombea maadui wake ju’ ya msalaba. Aliteswa kwa miiba, aliona maumivu. Ninaimba kwa furaha: “Yesu yeye yule leo!”

S.C. Kaufman, 1895
Have you ever heard the story, R.H. 442